Saturday, April 6, 2019

AMEZUILIWA ASIENDE KWENYE HATIMA YAKE

SIKU YA TANO YA SEMINA YA NENO LA MUNGU
KANISA LA UFUFUO NA UZIMA MOROGORO
PASTOR DR. GODSON ISSA ZACHARIA
ALHAMISI TAR O4 APRIL, 2019
MUHUBIRI: PASTOR PAUL JOSHUA (SNP KIGOMA)

Mchungaji Kiongozi Dr. Godson Issa Zacharia.

Mchungaji Kiongozi Paul Joshua (SNP KIGOMA)

UTAMGULIZI
Kwenye maisha yeyote mtu unayemuona yupo juu kuna mtu alimsaidia kumvusha ili aweze kwenda kwenye hatima yake. Wewe peke yako huwezi kwenda kwenye hatima yako hata kama umesoma, unaakili, unahela huwezi peke yako unahitaji mtu akuvushe. Hata Daudi kuwa mfalme alimuhitaji Samweli ampake mafuta ndipo awe mfalme. Pia Samweli ili awe nabii alimuhitaji Eli ampake mafuta hivyo katika maisha unamuhitaji mtu ili akusaidie kusonga mbele.
Kila mtu ana hatima yake yaani ana sehemu ambayo Mungu amempangia kwenda, kila aliyeokoka kuna sehemu ya maisha yake ambako anaelekea. Unaweza kuanzia chini kabisa lakini kuna sehemu Mungu anakupeleka na wakati Mungu anakupeleka huwezi kujua kama kuna sehemu unaenda lakini utaona mabadiliko katika maisha yako. Unaweza kuzaliwa kwenye nyumba ya majani lakini ukaishia kwenye ghorofa unachotakiwa kujua ni kwamba unapoanzia sio utakapo ishia. Sauli alianza na Mungu kama mtu aliyepoteza punda wa baba yake lakini katika kutafuta tafuta akaishia kwenye ufalme, Daudi alianza kwenye kuchunga kondoo wa baba yake lakini katika kuchunga kondoo akachaguliwa na Bwana kumuua Goriath na kisha akawa mfalme, ndugu yangu usidharau mambo madogo Mungu huwa anaanza na mambo madogo lakini baadae yanakuwa makubwa.
Jioni ya leo hii tamka ya kwamba hujafika yaabi hujafika mahali ambako unatakiwa kwenda ili umiliki hatima yako, hata maisha uliyonayo bado hujafika na ndio maana unaona shida, mateso, magonjwa na taabu, unaona kila ukijaribu kufanya biashara hufanikiwi kabisa kuna mtu umekwama sehemu ili usiende mbele lakini nataka kukwambia kuwa leo hii lazima uende kule ambako Mungu anataka uende. Wachawi wanaweza kuona unakoelekea, wanaweza kuona ndoa inapoelekea wanaweza kukuona kwamba huyu baba au mama leo kaanza kidogo lakini baada ya miaka mitatu minne utakuwa mtu fulani, unaanza kuonekana tangu ukiwa mdogo.
“Yesu alipozaliwa katika Bethlehemu ya Uyahudi zamani za mfalme Herode, tazama, mamajusi wa mashariki walifika Yerusalemu, wakisema, Yuko wapi yeye aliyezaliwa mfalme wa Wayahudi? Kwa maana tuliiona nyota yake mashariki, nasi tumekuja kumsujudia.” (Mathayo 2:1-2)
Watu walifunga safari kwenda kumtazama Yesu Mfalme wa wayaudi maana yake mtu anaweza kuonekana kwamba atakuja kuwa tajiri, kuwa kiongozi, kuolewa na mtu fulani mkubwa hivyo wachawi wakiona tu wanaamua kukuzuia. Shetani anafanya kila njia kupindisha hatima yako yaani ulikuwa na mikono ya fedha, ulikuwa na mambo mazuri, lakini leo hii umekwama unaona biashara haiendi kama zamani, unaona mambo hayaendi kabisa unajiuliza ni kwanini mbona zamani yalikuwa yanaenda lakini kumbe kuna wachawi wamekaa wakachungulia hatima yako na kuamua kukufunga ili kwamba usifanikiwe usiende kwenye mafanikio yako.
Kuna mtu mwingine kafungiwa kwenye nyumba ya majani ili kwamba asiende kwenye nyumba nzuri. Hakuna vita vikubwa kama mtu kuwa na kwake yaani vita vya ardhi au vita vya kumiliki ardhi. Kuna watu mpaka wanakufa hawajawahi kumiliki ardhi na ndio maana watu wanapigana kwa sababu ya ardhi huwezi kuwa tajiri kama huna ardhi, huwezi kumiliki kama huna arhi, utajiri wote umo ndani ya ardhi, madini, mazao, nyumba pamoja na vitu vizuri vyote vimo ndani ya ardhi.
Kuna watu wengi wamezuiliwa sana ili wasiweze kumiliki ardhi lakini leo hii ninatangaza kwenye ulimwengu wa roho mashetani wote waliokaa ili kukuzuia wewe usiende unapotakiwa kwenda leo hii ninawafyeka kwa jina la Yesu Kristo na ninafungua hatua zako tena umiliki kile ardhi tena na kujenga nyumba nzuri kwa jina la Yesu Kristo.
Kuna watu wanatakiwa kwenda kwenye nyumba zao lakini wamefungwa wasiende, mwingine hata ramani unayo kabisa lakini umefungwa miguu ili usiende kumiliki nyumba. Mwingine unaweza kuota ndoto kwamba miguu yako imekuwa mizito sana, mwingine unaota ndoto unatembea lakini miguu ni mizito sana yaani haufiki kule unapoelekea, mwingine unaota ndoto unapanda mlima lakini miguu yako ni mizito sana ukiona hivyo jua kuwa miguu yako imelogwa yaani umefungwa sehemu ili ushindwe kwenda kwenye hatima yako. Kuna kamba za wachawi, waganga, na mashetani zimekufunga ili usikimbie na ndio maana unaona mambo yako yanaenda polepole biashara inaenda taratibu unaweza kuona kuwa unaanza biashara na mtu mnaanza na mtaji sawa, mnaanza siku sawa lakini biashara yako ikawa inasuasua na ya mwenzako inaenda vizuri ni kwa sababu miguu yako imefungwa ili usiende.
Wachawi wanaweza kuona nyota yako, wanaweza kuona je hii nyota ni ya wapi, je ataishia wapi. Hata kwenye kazi ya Mungu kuna sehemu ya kufika ambayo Mungu amekuandalia ili ufike kama mtumishi wa Mungu Jehovah, aonavyo mtu nafsini mwake ndivyo alivyo hata mimi naona kuwa bado sijafika naona mbele kuna baraka zangu, mbele kuna mafanikio yangu, naiona huduma yangu mbele yangu inakwenda kustawi. Hata wewe katika maisha yako ifike wakati uanze kuona mabo mazuri yaliyo mbele yako, inatakiwa ifikie wakati uanze kuwa baraka kwa wengine yaani uwe na mali mpaka utoe kwa wengine, ifikie wakati uwe unamiliki nyumba mpaka unawabariki wengine, uwe na magari mengi mpaka mengine unatoa kwa watu, ifikie wakati uwe na vyakula vingi mpaka vingine unaamua kusaidia watu wengine.
Kila mtu anayo njia ya maisha yake ambayo Mungu amemuandalia ambayo kwa hiyo inakuongoza kuelekea kwenye hatima yako njema inaweza kuwa kwenye biashara yako, kazi yako, ndoa yako, kazi yako n.k. Siku moja nilimwomba Mungu anionyeshe njia ya maisha yangu nikafunga na kuomba mara ya kwanza nikaona magogo na miti mikubwa imezuia njia yangu, nikaomba sana tena kwa mara ya pili nikaona kwenye njia yangu kubwa kuna mtu mmoja mkubwa amekaa kwenye njia yangu mkubwa anatisha sana anasema kuwa huku huendi unaenda wapi mbona kwenye familia yako hakuna mtu aliyeenda huku kisha nikaona kamba zimenifunga miguuni nikasema kwa jina la Yesu kamba zikakatika katika miguu. Wakati huu nilikuwa katika maombi ya mfungo ndugu yangu nataka nikwambie kuna mambo mengine hayatoki bila kufunga na kuomba ukishinda kwenye kipengele cha kufunga yaani kuto kula pamoja na usingizi yaani kuamua kuto kulala ili uombe na ndipo mambo yako yatakapo kwenda sawa.
Kanisa likimtafuta Mungu hata mchungaji anapata unafuu wa kufungua kanisa, jifunze kuamka usiku anza kuomba mtafute Mungfu asipojibu leo atajibu kesho omba yafanye maombi kuwa sehemu ya maisha yako omba omba mpaka unazeeka mpaka unakufa omba mpaka unakata roho.
Kuna mtu leo hiii anatamani kujenga lakini hawezi ni kwa sababu katika ulimwengu war oho ame3fungiwa kwenye nyumba ya majani yaani anaishi kwenye kibanda kilichoezekwa kwa majani na ndio maana huna nyumba na huta weza kujenga kwa sababu ardhi imeambiw kuwa utangetange kwenye nyumba za kupanga mpaka ufekwa sababu kwenye adhi kuna mtawala. Wakati mwingine unaweza kufanikiwa kujenga nyumba lakini usikae kwenye hiyo nyumba aidha unaweza kufa au unaweza kukaa kwenye hiyo nyumba lakini ukawa hulali kila unapol,ala unaona kama nyumba inapanda juu na kushuka inakuwa ni mateso makubwa kwa sababu umezuiliwa ili usimiliki ardhi.


Baadhi ya makutano waliohudhuria semina ya Neno la Mungu lililofundishwa na Mchungaji Paul Joshua kutoka Kigoma.
Kuna watu ambao wanatakiwa kwenda kwenye hatima zao lakini wachawi wamewafunga miguu yao. miguu inaisha ray a kumiliki (Joshua 1: 3)… kila mahali mabako nyayo za miguu zikikanyaga tu panakuwa ni petu haijarishi amejenga nani, anakaa nani, kuna siri ya kumiliki mali za adui, kila kitu ambacho unakitafuta kuna mtu yupo hakuna kipya, unatamani uwe bosi ofisi Fulani tayari kuna bosi hivyo inatakiwa kusukumana tu yaani kumuondoa mtuj ili u7kae wewe, kuna mtu amekushikia gari lako, kiwanja chako, ofisi yako kinachotakiwa tu ni kumuondoa na kumiliki vitu vyako na leo hii nakufungfua miguu yako uende ukamiliki kazi yako, ndoa yako, ardhi yako n.k. nenda kwa jina la Yesu Kristo.
Kila sehemu ambayo uliwahi kuota ndoto kuwa umeenda lazima ufike ikiwa utapambana kumuondoa azuiaye kwa maana tayari umesha pamiliki mahali pale, mguu wako wa ndani amekwisha kufika imebaki tu wewe kwenda kimwili unatakiwa kupambana ili uende kwa jina la Yesu Kristo. Usikubali kufia jangwani kwa jina la Yesu Kristo.
Kuna wengine baraka zako zimo ndani ya wito; yaani ukiacha wito umeziacha baraka kuna mwingune unasikia kusaidia watu, kumtumikia Mungu n.k. ambacho Mungu amekuitia ndani yake kuna baraka yako, kuna kazi yako, ndoa yako, biashara yako n.k. ukitaka kuishinda vita kwa wepesi basi mtumikie Mungu ukimtumikia Mungu hata kama unadeki kanisa unaitwa ni mpaka mafuta wa Bwana, hata kama ni showers unakuwa ni masihi wa Mungu, hata kama ni muimbaji, muhubiri, au mpokea wageni kanisani unakuwa ni mpakwa mafuta wa Bwana hivyo mtu akikugusa anakuwa amegusa mboni ya jicho la Bwana hivyo anapondwa kabisa na wewe unakuwa huru.
Kuna watu ambao wanatamani sana kwenda kwenye hatima zao lakini wanashindwa kwenda mwingine miguu yao imefungwa na nyoka kabisa; nyoka amewafunga ili wasiende. Yaani unatamani kwenda mbali kimasomo lakini huwezi kwa sababu kuna kamba ambazo zimekufunga ili usiende, unaweza ukaona kuwa umempamtu mtaji.
Kuna wengine miguu yao ina mavazi ambayo imevikwa. Kuna mavazi ya kitajiri, maskini, kikuhani, vazi la heshima, vazi takatifu n.k. mwingine anatembea lakini rohoni hana nguo kabisa wamekwisha kunyang’anya vazi lako lakini njioni ya leo vazi lako litaonekana tena Yesu mwenyewe alivaa vazi ambalo lilikuwa na jina Mfalme wa wafalme kumbe kwenye vazi kuna jina. Kuna wengine hawana vazi la rohoni lakini leo hii Yesu anakwenda kukurudishia vazi lako kwa jina la Yesu Kristo.
Kuna vitu umepoteza yaani vitu vya rohoni umepoteza kama vazi, viatu vyako vya kiroho. Ukipoteza hivi unakuwa ni wakawaida kabisa yani hata hutishi wachawi hawakuogopi kabisa kwa sababu huna vazi na viatu vya rohoni. Viatu vya rohoni vinakusaidia wewe uweze kumiliki biashara, utajiri, afya, ardhi, viatu vinakusaidia umiliki huduma n.k. leo hii naifungua miguu yako iliyofungwa kwa jina la Yesu Kristo.
Kamba za kichawi zinaweza kumfunga mtu yaani anaweza kuanza biashara akafanya wewe lakini baadae ikafa kwa sababu miguu yake ya rohoni imefungwa ili asiende kwenye mafanikio. Mwingine kafungwa miguu yake yaani miguu imelogwa asiende mbali. Kuna mtu alitegewa uchawi njiani ukakanyaga na shida ikaingia kwenye maisha yako.
“Waitia miguu yangu katika mkatale, na kuyaaua mapito yangu yote; Wajiandikia alama kuzizunguka nyayo za miguu yangu” (Ayubu 13:27)
Miguu inaweza kufungwa na mikatare; hii ni aina ya kamba ngumu sana ambayo ikikufunga huwezi kupiga hatua kabisa. huwezi kupiga hatua kuelekea kwenye ushindi wako, utajiri wako lakini leo nakufungua na uwe huru kabisa kwa jina la Yesu.
DALILI ZA MTU ALIYEFUNGWA MIGUU YAKE ILI ASIENDE KWENYE HATIMA YAKE.
1. Miguu kuwaka moto
2. Miguu kuwasha
3. Miguu kuvimba; unaweza kuwaza ama ni presha au nini na miguu hii inavimba kwa muda fulani tu ambapo unatakiwa kwenda kwenye mafanikio yako. ukitaka kuanza biashara inavimba na ukisema kuwa basi naamua kukaa nyumbani basi miguu inapona kabisa. lakini leo hii ninaamuru kwenye ulimwengu wa roho kila kamba zilizoka kufunga miguu yako ili usiende leo hii ninazikata kwa jina la Yesu Kristo.
KWA MSAADA ZAIDI NA MAOMBEZI:
FIKA KANISANI,
KANISA LA UFUFUO NA UZIMA MKUNDI MINARA MITATU MOROGORO
AU WASILIANA NASI KUPITIA
FACEBOOK: Pastor Dr Godson Issa Zacharia
Follow us on INSTAGRAM: pastordrgodson
Follow us on YOUTUBE: Pastor Dr. Godson Zacharia


TEL: +255 719 798 778
Share:

Sunday, June 10, 2018

SOMO: NINAKATAA UDHAIFU NA MAGONJWA YA KISHETANI


GROLY OF CHRIST TANZANIA CHURCH (GCTC)
KANISA LA UFUFUO NA UZIMA -MOROGORO
PASTOR DR. GODSON ISSA ZACHARIA

JUMAPILI 10 JUNE, 2018

“Bwana ni nuru yangu na wokovu wangu, Nimwogope nani?, Bwana ni ngome ya uzima wangu, Nimhofu nani? Watenda mabaya waliponikaribia, Wanile nyama yangu, Watesi wangu na adui zangu, Walijikwaa wakaanguka”
Zaburi 27:1-2

UTANGULIZI;
Magonjwa na udhaifu wowote unao ufahamu na usioujua hautokani na Mungu,. Asili ya magonjwa na udhaifu ni ulimwengu wa roho (yaani mashetani). Kuna watu wanawaza magonjwa, shida na udhaifu ni mambo ya kibaolojia, si kweli! Ukijua vizuri na kumpiga anayaeleta udhaifu na magonjwa utakuwa salama.
Kupitia SOMO hili utajifunza namna shetani anavyoleta udhaifu kwenye maisha ya watu na jinsi ya kuyakataa ili uwe huru kwa jina la Yesu.

Ninaposema magonjwa na udhaifu simaanishi magonjwa na udhaifu wa mwilini tu, bali magonjwa na udhaifu wa vitu mbalimbali mfano udhaifu kwenye mambo ya fedha, akili, tabia, mambo ya ndoa n.k;
Mfano; mtu anaweza kuwa na udhaifu wa kihisia, akipanda kwenye daladala nilazima amtongoze jirani yake hata kama hajuhi ni mke wa mtu au ni mgonjwa. Mwingine anaweza kuwa mdhaifu kwenye pombe, akisikia harufu ya pombe anakosa amani. Udhaifu huu unatengenezwa na mashetani ili wewe uachwe, usipige hatua, leo Bwana anataka useme kwa kinywa chako kuwa NAKATAA magonjwa, NAKATAA udhaifu wa kishetani kwa jina la Yesu.
Kuna nguvu katika kukataa, Raila Odinga alikataa kukubali matokeo ya uraisi, na alilopokataa akawekwa pamoja na raisi madarakani. Ulipoumbwa Mungu hakukuumba uwe mlevi, mchoyo au kilema, shetani ameandaa udhaifu na magonjwa ili afya, kazi, ndoa iharibike. Kama shetani alikuwa ameandaa udhaifu wewe ukianza kukataa udhaifu, magonjwa mara kwa mara mletaji anayabeba na kuyapeleka mahali pengine.
Ikiwa Bwana ni nuru ya wokovu wetu, je twaweza kuwaogopa wachawi, wasoma nyota, waganga? Hapana! Ikiwa watenda mabaya wamekuja kukutesa, wakiwa wamebeba magonjwa na udhaifu wa kila aina ya mateso, waje kula nyama yako, kukuangamiza wewe USIOGOPE!! kwa maana Mungu tunayemtumikia yu ndani yetu. Mungu yuko kila mahala, kazini, porini, ukiamini haya kuwa yeye ni mwokozi na mtetezi wetu hutaogopa maisha ni mwako.
“Bwana ni nuru yangu na wokovu wangu, Nimwogope nani? Bwana ni ngome ya uzima wangu, Nimhofu nani? Watenda mabaya waliponikaribia, Wanile nyama yangu, Watesi wangu na adui zangu, Walijikwaa wakaanguka. Jeshi lijapojipanga kupigana nami, Moyo wangu hautaogopa. Vita vijaponitokea, Hata hapo nitatumaini.Neno Moja nimelitaka kwa Bwana, Nalo ndilo nitakalolitafuta, Nikae nyumbani mwa Bwana Siku zote za maisha yangu Niutazame uzuri wa Bwana, Na kutafakari hekaluni mwake.Mradi atanisitiri bandani mwake siku ya mabaya, Atanisitiri katika sitara ya hema yake, Na kuniinua juu ya mwamba.” Zaburi 27:1-5
Duniani kuna mashetani ambao kazi yao ni kukukaribia ili wale nyama yako, kula ndoa yako, elimu yako n.k. Wakotayari kukutia udhaifu, wale mnofu wa biashara yako lakini Biblia inasema hata kama watakuja kukukaribia ukiwa na Yesu wao watajikwaa, kwa maana Yesu anaitwa jiwe likwazalo.
Shetani akimwona mtu ana mafanikio anatuma majeshi yake, akiona ameshindwa, anatuma wenye mamlaka kwenye ulimwengu wa roho, akishindwa analeta wakuu wa giza (Waefeso 6:12), anajipanga na majeshi aje akudhuru, wakati anaandaa jeshi ili kukudhuru Mungu naye anaandaa jeshi la kukulinda. Yawezekana yapo majeshi ya kishetani yamejiandaa kukuua wewe na maisha yako lakini leo naamuru jeshi la Bwana likae, likulinde wewe na familia yako kwa jina la Yesu.
Hii ndio siri tunayoijua sisi tunaomjua Bwana, mashetani wanafanya kazi pasipo kujulikana, kwa akili ya mbinguni tunafahamu kuna waanao taka kula nyama, hivyo wanajipanga kukuharibu. Tunalo jeshi la Bwana linatulinda, unaweza kutumiwa jeshi ili kuangamiza kazi yako, waue ndoa yako n.k. Mashetani wakimtia mtu udhaifu wao wanachukua wanacho kitaka kutoka kwake.

Asili ya magonjwa na udhaifu unaousikia duniani chanzo chake ni mashetani, katika ulimwengu wa roho. Baadhi ya watu wanawaza hivi magonjwa, shida na udhaifu ni mambo ya kibaologia si kweli wanasema mtu anaugua kansa kwa maana kuna wadudu fulani wameingia. Lakini tabu, shida na magonjwa vyote huanzia kwenye ulimwengu wa roho. Na si tatizo la kibailojia tukijua vizuri na kumpiga anayaeleta tutakuwa salama.
Lakini ikiwa huamini hivyo, ukiumwa kitu ukasema niende kwa daktari yeye atakata vidole vyako kwa sababu ya kansa, ni kweli madakarii wanafanya kazi lakini wewe kabla hujaenda kwa daktari omba kwanza. Ukiomba Yesu akikaa ndani yako wanapokukabiria wanijikwaa wanashindwa kuleta hayo magonjwa na udhaifu.
Mfano shetani anaweza kwenda kwa mtu kuweka udhaifu wa kichwa, mtu anaanza kuugua presha, anakunywa kila dawa lakini maumivu yako palepale, akidhoofika anakuja mwingine mla nyama, wanambeba wanamchukua msukule wengine wanajua kuwa amefariki kumbe amemchukuliwa na chanzo kimeanza rohoni ndo maana limeshindwa kutibika.
Mtu anaweza kuugua kansa lakini nyuma yake kukawa na roho ya kichawi, Dr. Robert Galo mwanasayansi wa Marekani, aliyetengeneza virusi vya UKIMWI alipomaliza akasema, “I have created HIV Aids in order to depopulate black people” nimetengeneza virus vya ukimwi ili kuwapunguza waafrika. Lakini wengine wanaita ugonjwa wa kisasa. Wachawi wanaweza kutengeneza udhaifu ili wapigane na wewe ili ushindwe, ushindwe kuanza kazi, ushindwe kuomba ndio maana lazima ukatae kwa jina la Yesu.
Magonjwa na udhaifu wote hautokani na Mungu, ukiona unaharisha, mgonjwa au mdhaifu hayo yote hayatokani na Mungu. Raisi wa Zambia alipoona kuna shida ya kipindupindu nchini mwake aliita watu wote waombe hadi kipindupindu kiishe. Magonjwa hayatokana na Mungu wala Mungu hawezi kukuwekea magonjwa au udhaifu ili akujaribu wewe. Ikiwa yatokana na Mungu kwa nini asikujaribu kwa kukupa fedha kuona kama utatoa sadaka au zaka, wengine wanasema ni mitihani ya Mungu, je nani anasahihisha mitihani hiyo?.
Magonjwa au udhaifu vinatokana na shetani, moyo wa Mungu hapendi kumtesa au kumuhuzunisha mwadamu. Mtu yoyote mwenye udhaifu na magonjwa hana furaha na Mungu amesema hapendi kumuhuzunisha mwanadamu, Yule mwanamke aliyetokwa na damu alikuwa na huzuni nyingi na kuteseka, na Mungu ameahidi kutomuuzunisha mwanadamu hivyo mateso yanatokana na shetani.
“Maana ajapomhuzunisha atamrehemu, Kwa kadiri ya wingi wa huruma zake. Maana moyo wake hapendi kuwatesa wanadamu.Wala kuwahuzunisha.” Maombolezo 3:32-33
Vipo vitu vinaleta huzuni, kuna mambo ulikuwa unafanya lakini hufanyi tena, kazi ulikuwa unafanya lakini hufanyi tena, husomi, huwezi kutembea n.k. Ndio maana Yesu alipokuja duniani alisema alikuja kuleta uzima na kuchukua huzuni zetu yeye akiona husomi, huzai, hufanyi kazi anapata huzuni ili akupe furaha, huzuni si sehemu ya Mungu kabisa.
“Alidharauliwa na kukataliwa na watu; Mtu wa huzuni nyingi, ajuaye sikitiko; Na kama mtu ambaye watu humficha nyuso zao, Alidharauliwa wala hatukumhesabu kuwa kitu.” Isaya 53:3
Kwa Mungu ukionekana una matatizo ni huzuni, lakini kwa shetani ukionekana una udhaifu na huzuni nyingi kwakwe ni furaha, cha ajabu watu wakimwona mtu anaukimwi au kisukali, au kansa wanasema ni mapenzi ya Mungu.
Je, umeteseka? Je, una huzuni ? Je, una huzuni? Ikiwa una hali kama hizo ujue ni shetani amekuletea hali hiyo, Mponyaji Mungu hawezi kutia magonjwa, hakuna mahala aliposema kuwa yeye ni Mungu wa kutia udhaifu.
"akawaambia, Kwamba utaisikiza kwa bidii sauti ya Bwana, Mungu wako, na kuyafanya yaliyoelekea mbele zake, na kutega masikio usikie maagizo yake, na kuzishika amri zake, mimi sitatia juu yako maradhi yo yote niliyowatia Wamisri; kwa kuwa Mimi ndimi Bwana nikuponyaye. " Kutoka 15:26
Wakati mwingine shetani anakuletea magonjwa na udhaifu kwa njia ya akili sana, anaweza kukuletea udhaifu kama zawadi, kama chakula, kama pongezi , ni wakati wako sasa kukataa, ukisema kabisa nakataa udhaifu, nakataa balaa, vinaondoka kwa jina la Yesu.
Siku moja shetani alienda mbele za Mungu, Mungu akamuuliza shetani unatoka wapi?, akasema natoka kuzunguka huku na huku (sawa na kusema nilikuwa kugawa vifurishi vya udhaifu dunia, lakini kuna kajamaa kamoja kanaitwa Ayubu kamekataa kupokea kifurushi cha udhaifu). Baada ya shetani kuharibu vitu vyake akawa anamtafuta yeye, ndipo akampiga Ayubu kwa majipu mwili mzima.
“Bwana akamwuliza Shetani, Je! Umemwangalia huyo mtumishi wangu Ayubu? Kwa kuwa hapana mmoja aliye kama yeye duniani, mtu mkamilifu na mwelekevu, mwenye kumcha Mungu na kuepukana na uovu; naye hata sasa anashikamana na utimilifu wake, ujapokuwa ulinichochea juu yake, ili nimwangamize pasipokuwa na sababu. Shetani akamjibu Bwana, na kusema, Ngozi kwa ngozi, naam, yote aliyo nayo mtu atayatoa kwa ajili ya uhai wake. Lakini sasa nyosha mkono wako, uuguse mfupa wake na nyama yake, naye atakukufuru mbele za uso wako. Bwana akamwambia Shetani, Tazama, yeye yumo mkononi mwako; lakini tunza tu uhai wake. Basi Shetani akatoka mbele za uso wa Bwana, akampiga Ayubu na majipu mabaya tangu wayo wa mguu hata utosi wa kichwa.” Ayubu 2:2-7
Shetani akikutembelea anakuja na kifurushi cha kuua, kuiba na kuharibu. (Yohana 10:10) akikuta huna wigo wa kimungu anakurushia kifurushi cha magonjwa, cha udhaifu, na aikisha kutia udhifu anakula nyama yako, anakuchukua mzima mzima, anachukua ndoa yako, kazi yako na kila ulicho nacho. Unapoona mwanzo ulikuwa sawa lakini gafla huko vibaya ujue kuna kifurushi cha udhaifu kimeletwa juu yako na shetani.
Ikiwa umezingirwa na wigo wa Mungu shetani hawezi kukudhuru kwa jambo lolote, atakapojaribu kula nyama yako anakuta umezingirwa wewe na mambo yako anashindwa kukuingilia. Ukimwona mume wako amepatwa na shida usimkimbie kama alivyofanya mke wa Ayubu mara nyingine ni shetani. Leo Bwana akuwekee ulinzi wa kimungu kwenye afya yako, kazi, watoto na mali yako na kila ulichonacho kwa jina la Yesu.
Kabla hujaenda hospitali omba kwanza, kuna magonjwa mengine ambayo njia za kidaktari hayawezi kutibika kwamaana chanzo cha magonjwa hayo ni rohoni yaani ya kichawi hayatokani na kibailogia kama watu wanavyo waza. Ndio maana Yesu Kristo alikuja kuleta uzima, yeye ambaye ni mfalme, aliyekuwako na Mungu akapigwa mijeredi ,ili kwakupigwa kwake sisi tupate uzima.
“Hakika ameyachukua masikitiko yetu, Amejitwika huzuni zetu; Lakini tulimdhania ya kuwa amepigwa, Amepigwa na Mungu, na kuteswa.” Isaya 53:4
Ikiwa umeamini kwamba Bwana hawezi kukukuhuzinisha ni rahisi kwako kukataa magonjwa na udhaifu wa kichawi. Biblia inasema Yesu alinyenyekea hata mauti , na kwakuwa alinyeyekea Mungu alimkilimia jina lipitalo majina yote ili kwa jina la Yesu kila goti lipigwa la vitu vya duniani na mbinguni. Jina la Yesu ni zaidi ya ukimwi, ni zaidi ya kansa, ni zaidi ya kifua kikuu. Ukiliamini jina la Yesu unashinda udhaifu wowote,
Shetani anaweza kuweka udhaifu kwenye kazi, ndoa, biashara yako na wewe ukaridhika. Biblia inasema lifanyeni kila jambo kwa jina la Bwana. Ukitumia jina la Yesu lenye nguvu, kwa jina la Yesu mashetani, udhaifu, magonjwa, kuzimu, inapiga magoti.
Injili ya Kristo inazungumza kwamba Yesu alifanya kazi kubwa ya kuwaondoa mapepo kwamaana kuna mahusiano kati ya mapepo na udhaifu na magonjwa, alishughurikia vitu vya rohoni ingawa alikuwa katika mwili, hakuja kutengeneza hospitali ya kansa, au kufungua hospitali ya watoto, au ya moyo, au benki ya fedha kwa maana alijuakuwa haya matatizo waliokuwa nayo wanadamu yanasababishwa na mambo ya kiroho
Siku moja alikwenda nyumbani kwa Petro akamkuta mkwe wa Petro hajiwezi kwakuwa alikuwa na homa, ndipo Yesu akamgusa mkono na homa ikamwacha akamtumikia. Wapo watu wamepata homa za kichawi na wamekuwa hawawezi, hawawezi kufanya kazi, hawawezi kusoma n.k lakini kwa jina la Yesu homa zinatoka na hao wanakuwa wanaweza tena kwa jina la Yesu.
“Hata Yesu alipofika nyumbani kwa Petro, akamwona mkwe wa Petro, mamaye mkewe, amelala kitandani hawezi homa. Akamgusa mkono, homa ikamwacha; naye akaondoka, akawatumikia.” Matahayo 8:14-15
Kuna vitu vinaweza kukufunga kisha ukawa dahifu, huwezi.. Unaweza kupatwa na homa ya kishetani ukawa huwezi, unaweza kukaliwa na pepo miguu ukawa huwezi kutembea, unaweza kufungwa mikono kichawi ukawa huwezi kushika, unaweza kufungwa mwili na kugeuzwa kila kitu chako na ukawa huwezi. Lakini pepo huyo akiondolewa unaweza tena kwa jina la Yesu. Ndio maana homa nyingine zina majina ya ajabu kama vile homa ya manjano, homa ya kuku, homa mafua,n.k kumbe ni pepo kazi yake ni kumfanya mtu asiweze.
Mambo tunayo yafanya katika dunia ya kawaida ni ya kibinadamu, kuna namana nyingine tumijiita majina mengi kama vile, siwezi kula, siwezi kusoma, siwezi kuona n.k. Neno hili limekuja baada shetani kutawala, limekuja baada shetani kuweka udhaifu kwenye maisha ya wanadamu. Yesu alikuja kuwaaondoa mashetani ya kutoweza
Injili ya Yesu inasema yeye alikuja kuwaondoa mapepo hili watu waweze, wazae, wafanye kazi, wafanye biashara wawe na afya njema. Wapo watu hawawezi kukaa na mke au mume pamoja kumbe ni mapepo yametengeneza kitu kwenye familia hata wanaonana kama mtu na dada, yakiingia mtu hatamani kufanya kazi tena, hawezi kujishughuisha kabisa.
Yesu alitembea mahala pote hata Galilaya akiwatoa watu mapepo na kuwaponya. Shetani amepanda vitu kwenye maisha ya watu lakini yeye alikuja kuvitoa, alipita kila mtaa na miji, ili aondoe udhaifu huo. Ndio maana kila pando lisilopandawa na Baba wa mbinguni litangolewa.
“Naye alikuwa akizunguka katika Galilaya yote, akifundisha katika masinagogi yao, na kuihubiri Habari Njema ya ufalme, na kuponya ugonjwa na udhaifu wa kila namna katika watu. Na habari zake zikaenea katika Shamu yote; wakamletea wote waliokuwa hawawezi, walioshikwa na maradhi mbalimbali na mateso, wenye pepo, na wenye kifafa, na wenye kupooza; akawaponya.” Mathayo 4:23-24
Kuna mtu amewekewa udhaifu kwamba hawezi kujibidiisha, hawezi kutafuta kazi, hawezi wala kufanya kazi, tangu asubuhi ameshinda anaangalia Tv kwamaana amewekewa roho ya kutoweza, kuna watu hata kusema nakupenda kwa mke wake ni mwiko, unatakiwa sasa uondoe hali ya kutoweza maisha mwako kwa njia ya kukataa kwa jina la Yesu,
Mungu amekuweka juu ya mataifa na falme ili kung’oa mapando ya kishetani ili uwe huru kwa jina la Yesu. Yesu alaitembea miji na vijiji akifundisha na kuwatoa watu mapepo kuwatoa katika hali ya kutoweza, na baada ya kazi yake aliwatuma wanafunzi kuifanya kazi yake aliyoianzisha, wewe unaye mwamini Yesu unaweza kuponya magonjwa na udhaifu wa kila namna.
“Akawaita wanafunzi wake kumi na wawili, akawapa amri juu ya pepo wachafu, wawatoe, na kupoza magonjwa yote na udhaifu wa kila aina.” Mathayo 10:1
Wachawi, mapepo, waganga kazi yao kubwa ni kuleta udhaifu na magonjwa kwenye maisha ya wanadamu. Yakitolewa mtu anakuwa salama kwa jina la Yesu. Siku moja Yesu aliletewa mtu mwenye kifafa, aliyekuwa anamwangusha kwenye moto, kwenye maji, Kuna mahusiano makubwa kati ya mapepo na kuanguka kwa Yule kijana, na mapepo yalipo mtoka akawa salama.
“Naye Yesu akiona ya kuwa mkutano unakusanyika mbio, akamkemea yule pepo mchafu, akamwambia, Ewe pepo bubu na kiziwi, mimi nakuamuru, mtoke huyu, wala usimwingie tena. Akalia, akamtia kifafa sana, akamtoka; naye akawa kama amekufa; hata wengi wakasema, Amekufa. Lakini Yesu akamshika mkono akamwinua naye akasimama.” Marko 9:25-27
Ni sawa na wewe uliyetembea kila mahala na kuingia kila hospitali lakini ujapata nafuu, ni wakati wako sasaa kuja kwa Yesu kugusa pindo la vazi lake ili upate uponyaji, ukigusa pindo la vazi la Yesu unapata uzima, udhaifu unaondoka, nawe unakuwa huru kwa jina la Yesu.
Jifunze kuomba, protokali za kidunia ziache ziende lakini mtu anaye mtumikia Mungu lazima uombe, unakataa magonjwa, unakataa udhaifu wako na wafamilia yako, ukikataa kwa maombi udhaifu wowote ule unaondoka kwa jina la Yesu. Nivizuri ujifunze kuomba (Tafuta kitabu cha KUOMBA KWA BIDII KILICHOANDIKWA NA PASTOR, DR. GODSON ISSA ZACHARIA, kwa msaada wa kujifunza kuomba) ukiwa ni mtu wa maombi shetani hawezi kukushinda.
Ukitaka kutoa tatizo maishani usishughurike na matawi ya tatizo lako, bali shughurika na chanzo cha tatizo lako, ikiwa mizizi ya tatizo lako ikiisha unakuwa salama, Yesu aliletewa shida ya kifafa lakin chanzo cha shida hiyo ilikuwa ni mapepo
Pepo anaweza kumfanya mtu atokwe na povu, asage meno, lazima utumie mamlaka na uwezo wa kutoa mapepo hayo. Nguvu hizi zinatokana na kumpokea Yesu, lazima umkiri Yesu kuwa Bwana na mwokozi wake, na kumwamini moyoni mwake utaokoka. Kuoka si baadaye, au hakupo, wokovu ni sasa.
Mungu alikuja kutafuta na kuokoa kilichopotea akikuokoa wewe anakuokoa wewe na mambo yako yote, kukiri kunasababisha mtu kufanyika mtoto wa Mungu, ukifanya hivyo unahama ufalme kutoka ufalme wa giza kuingia wa ufalme wa nuru, ndio sasa unapata uwezo wa kumshinda adui shetani kwa jina la Yesu.
“Kwa sababu, ukimkiri Yesu kwa kinywa chako ya kuwa ni Bwana, na kuamini moyoni mwako ya kuwa Mungu alimfufua katika wafu, utaokoka. Kwa maana kwa moyo mtu huamini hata kupata haki, na kwa kinywa hukiri hata kupata wokovu.” Warumi 10:9-10

KWA MSAADA ZAIDI NA MAOMBEZI:
FIKA KANISANI,
KANISA LA UFUFUO NA UZIMA MKUNDI MINARA MITATU MOROGORO
AU WASILIANA NASI KUPITIA 
FACEBOOK: Pastor Dr Godson Issa Zacharia
Follow us on INSTAGRAM: pastordrgodson
Follow us on YOUTUBE: Pastor Dr. Godson Zacharia
TEL: +255 719 798 778
BLOG: Ufufuo na Uzima Morogoro
Share:

Sunday, May 20, 2018

OPARESHENI YA KUTAFUTA NA KUOKOA KILICHOPOTEA


  
GROLY OF CHRIST TANZANIA CHUCH (GCTC)
KANISA LA UFUFUO NA UZIMA –MOROGORO
PASTOR DR. GODSON ISSA ZACHARIA

JUMAPILI MAY 20, 2018


Mchungaji Kiongozi Dr. Godson Issa Zacharia akiwa tayari kutafuta na kuokoa kilichopotea.



UTANGULIZI
Kwa miaka mingi jamii za watu, kabila na lugha wamekuwa chini ya utumwa wa shetani, maisha yao yakiongozwa naye. Wametawaliwa kimwili na kiroho, wamenaswa kwenye mashimo, wamekuwa mawindo, wamezamishwa kwenye misitu ya uovu, wameibiwa mali na vitu vyao na wamekosa msaada, lakini Mungu kwa upendo wake akamtoa mwanae mpenzi ili watu waokolewe. Kwakuwa Mwana wa Adamu alikuja kutafuta na kuokoa kile kilichopotea.

“Kwa kuwa Mwana wa Adamu alikuja kutafuta na kuokoa kile kilichopotea.” (Luka 19:10)

Mwana wa Adamu ni Yesu Kristo mwenyewe (Yoh 1: 14). Hapo mwanzo Yesu alikuwa ‘Neno’, alikuwa kwa Mungu, naye ‘Neno’ akavaa mwili akakaa kwetu (Yohana 1:1-3).  Ndiye aliyekuja kama Imanueli [Mungu pamoja nasi] akazaliwa na mwanamke, akautoa uhai wake ili kupitia huo awaokoe wanadamu ambao ni mimi na wewe kutoka katika mikono ya shetani.
Baadhi ya makutano haya wakifuatilia neno la Mungu kuhusu Oparesheni kutafuta na kuokoa kilichopotea

Yesu Kristo alizaliwa kama mwanadamu wa kawaida, aliishi kama mwanadamu wa kawaida. Ulipofika wakati wake wa kuitenda kazi ya Mungu aliingia hekaluni, akisha kupewa kitabu,  akafungua unabii uliokuwa umetabiliwa na nabii Isaya, akasoma maandiko yafuatayo kudhihilisha lile alilojia hapa dunia.
“Akapewa chuo cha nabii Isaya, akakifungua chuo, akatafuta mahali palipoandikwa, Roho wa Bwana yu juu yangu, Kwa maana amenitia mafuta kuwahubiri maskini habari njema. Amenituma kuwatangazia wafungwa kufunguliwa kwao,  Na vipofu kupata kuona tena, Kuwaacha huru waliosetwa,Na kutangaza mwaka wa Bwana uliokubaliwa.  Akakifunga chuo, akamrudishia mtumishi, akaketi; na watu wote waliokuwamo katika sinagogi wakamkazia macho. Akaanza kuwaambia, Leo maandiko haya yametimia masikioni mwenu.”  (Luka 4:17-21)

Maneno ya Bwana huwa yana andikwa na kutunzwa kwa wakati wake, ukifika wakati wa utimilifu wa maneno hayo matakatifu ya Mungu, Mungu humtuma mjumbe wake kuyatimiza. Unabii wa nabii Isaya uliandikwa miaka mingi sana iliyopita, lakini wakati wa kutimia kwake ulikuwa hujafika bado, ndipo Kristo alizaliwa baada ya muda kutimiza unabii huo.
“Roho ya Bwana MUNGU i juu yangu; kwa sababu Bwana amenitia mafuta niwahubiri wanyenyekevu habari njema; amenituma ili kuwaganga waliovunjika moyo, kuwatangazia mateka uhuru wao, na hao waliofungwa habari za kufunguliwa kwao. Kutangaza mwaka wa Bwana uliokubaliwa, na siku ya kisasi cha Mungu wetu; kuwafariji wote waliao;” (Isaya 61:1-2)

Tangu wakati wa nabii Isaya watu walikuwa wanachukuliwa mateka, waliwekwa chini ya utawala wa giza na kumezwa na mwovu pasipo msaada wowote. Ndipo mwana wa Adamu akaja duniani kutafuta na kuokoa kile kilichochopotea, kuwafungua waliofungwa na kuonewa chini ya utawala shetani Ibilisi.

Yesu anapokuja kutafuta kwenye maisha ya wanadamu, huwa hatafuti lile linalo onekana, hutafuta ambalo limepotea, limefichwa, limeibiwa na kuwekwa mahali pa siri. Ikiwa kuna kitu ambacho ulikiweka mahali fulani ukategemea kesho ukichukue na ulipoenda siku inayofuata ukakikosa ujue kuwa kimeibiwa. Mungu aliwaweka wanadamu duniani wakiwa kamili, lakini watu hao wamepotea, wamepoteza mali zao, ndoa, mazao yao yameibiwa na kufichwa mahali. Ndipo sasa Mungu akaja ili kuokoa na kutafuta kilichopotea.

Baadhi ya Makutano wakijifunza kwa habari ya kutafuta na kuokoa kilichopotea.

Bwana uingia kwenye mashamba, kwenye mapori, mapango, nyumba za watu, juu ya dali. kwenye ofisi za watu, n.k, kutafuta na kuokoa kile ambacho kimeibiwa na kufichwa mahali. Yapo mambo mengi na vitu vingi vyako vimehamishwa mahali pake na kupelekwa sehemu nyingine. Mfano, amani yapasa kuwako ndani ya ndoa na familia lakini inaibiwa na kufichwa mahali hatimaye ndoa imekua uchungu, ndipo sasa anakuja kuitafuta ili kuirudisha mahali pake. Mchungaji mwema akiwa amepoteza kondoo mmoja ndani ya kundi la kondoo mia, huwaacha hao tisini na kenda na kuenda kumtafuta mmoja aliyepotea na akisha mpata anafurahi sana.

Biblia inataja habari za Mwana mpotevu aliye omba mali na fedha kutoka kwa baba yake , kwa kuwa baba yake alimpenda akampa, akenda nchi ya mbali, akatapanya mali hizo kwa uzinzi na uasherati. Njaa ikaingia kwake hata akaamua kujilisha pamoja na nguruwe, kwa mateso hayo akapata akili na akawaza kurudi kwa baba yake, aliporudi baba yake akafurahi sana kwa kumuona mwanae, (Luka 15:11-20). Hakika kuna furaha katika kurudisha, leo Bwana anataka kuokoa na kurudisha vitu vyako vilivyofichwa na mwovu kwa jina la Yesu.

Biashara yako iliyokufa, kazi yako iliyokufa, elimu iliyokufa, Bwana amekuja kuiokoa na kuirudisha mahali pake. Mara nyingine unajikuta wewe ni mama, siku zako zimepotea; mwezi wa kwanza, wapili hata watatu yamkini wamezipoteza ili hukose mtoto. Yesu Kristo amekuja ili urudishe kile ulichopoteza kwa jina la Yesu.

Macho ya Mungu yanaona kila mahali, huenda ukawa umechukuliwa kwa namna ya rohoni na kuweka kwa siri kwenye mkoba wa mtu, kwenye uvungu wa mtu. Mara nyingine unaweza kuibiwa na kuchukuliwa vitu vyako halali na kuwekwa mahali. Mfano, unaweza kuibiwa soksi moja ikapelekwa mahali na tangu siku hiyo umekuwa unatabia mbaya, mambo hayaendi kwakuwa umechukuliwa kwa namna ya kichawi.

Platform wakiongoza kipindi cha sifa na kuabudu.

Nguo, nywele, kucha au kitu chako chochote ni kiwakilishi chako. Yusufu alipomkimbia mke wa Potifa aliacha sharti, na kupitia sharti hilo alikamatwa na kuweka gerezani. Hivyo mali yako au sehemu yako inaweza kuchukuliwa na watu waovu ikapelekwa mahali na ikawa kiwakilishi chako katika kutesa maisha yako yote. Leo Bwana anataka kurudisha kile kilicho ibiwa, kurudisha kazi, ndoa,n.k.  kwa jina laYesu.

Akili ya mtu pia inaweza kuibiwa, kutekwa, upendeleo wako unaweza kuchukuliwa, kibali chako kinaweza kutekwa mahali ili tu uharibikiwe. Kwakuwa Yesu alifahamu haya ndipo akaja kutafuta na kuokoa kile kilicho potea.

Mtu aweza kuchukuliwa na kutekwa, mali na mambo yako yanaweza kuchukuliwa na kutekwa. Vile vitu vyako vinavyo haribika mara kwa mara ni kwasababu kunamtekaji amekuja kuvichukua na kuviteka. Mtu anapochukuliwa mateka, na kwakuwa mtu huyo huwa haonekani wanamwita msukule na mara nyingi huwa anakufa kabisa katika hali ya mwili na ndipo wanamchukua na kumteka anakosa uhuru, na utumiwa kama anavyotaka mtekaji wake kwakukosa maarifa.
“Kwa sababu hiyo watu wangu wamechukuliwa mateka, kwa kukosa kuwa na maarifa; na watu wao wenye cheo wana njaa, na wengi wao waona kiu sana.” (Isaya 5:13)

Nabii Isaya alionyeshwa na Mungu kwamba watu hawa wanao onekana; wanakula, wanatembea, walala na kumka, kuoa na kuolewa, wameibiwa na kutekwa, wamechukuliwa na kunaswa kwenye mashimo. Chanzo kikubwa cha kuchukuliwa kwao ni kukosa maarifa, kutokujua kamaa kunawachawi, kuna waganga, majini. Kushindwa kufahamu kuwa kwa jina la Yesu ataokolewa. Shetani siku zote anafanya kazi kwa siri sana ili asionekane, anapata nguvu ikiwa anachomfanyia mtu hakijulikani.
“Lakini watu hawa ni watu walioibiwa na kutekwa; wote wamenaswa katika mashimo, wamefichwa katika magereza; wamekuwa mawindo, wala hapana aokoaye; wamekuwa mateka, wala hapana asemaye, Rudisha.” (Isaya 42:22)

Shetani alijaribu kumwibia Ayubu mali, ndoa, kazi zake akashindwa kwakua Bwana alimzingira Ayubu pande zote kwamaana alimtumikia Mungu kwa mwaminifu (Ayubu 1:1-3). Ndipo shetani akaenda mbele za Mungu akamwambia atoe mikono yake ya ulinzi kwa Ayubu (Ayubu: 10), Mungu alipotoa mikino ndipo mambo yakaharibika, mali zikaharibika na kila alichokuwa nacho (Ayubu 1:13-20).  Watoto wa Ayubu na mali zake ziliibiwa na watu au mipango ya shetani si kwaajili ya Mungu. Kuna wakati shetani anavaa mwili akatenda kazi kama binadamu ili aibe mali na vitu vya wanadamu.

Maranyingine waweza kumuona mtu mwenye afya nje, cheo na mali lakini ametekwa, ameibiwa fedha, mali, kazi n.k. Wamefungiwa huko hata hawawezi kujiongoza wenyewe, wamewekwa kwenye nguvu za shetani na utawala wake hata hakuna msaada. Wakati mwingine mtu anaweza kuibiwa tumbo, akili, moyo n,k vikawekwa mahali kifungoni.
Baadhi ya Makutano waliamua kumpa Yesu maisha yao ili waweza kutafuta, na kuokoa kilichopotea.

Unaweza kuibiwa sura yako au akili yako. Wanaenda  kwa waganga nakuchukua kile wanacho kitaka kwako, sasa yule aliye ibiwa anakuwa katika kundi la kukataliwa, hakuna anaye msemesha, hakuna anaye mtaka kwakuwa sura au kibali chake kimeibiwa. Leo Bwana arudishe kibali chako kwa jina la Yesu.

Jambo la kushangaza chini ya nchi nikuwa wale walio ibiwa na kutekwa ni wengi sana kuliko walio huru. Mtumishi wa Mungu Stephano alipigwa kwa mawe hadi kufa (Matendo 7:59), wengine walichomwamoto, na kukatwa vichwa (Marko 6:24-25). Kimsingi si wote wanaokufa, wanaopotea, wanaokaa kifungoni ni mapenzi ya Mungu, hapana! ni kazi za wovu. Ndipo bwana anasema siwezi kukaa ikiwa watu wake wanatekwa, wanauawa, wanapelekwa utumwani ndipo akasema.
“basi sasa, nafanya nini hapa, asema Bwana, ikiwa watu wangu wamechukuliwa bure? Hao wanao watawala wanapiga yohe, asema Bwana, na jina langu linatukanwa daima mchana kutwa”(Isaya 52:5)

Mwanadamu ni kazi ya Bwana, lakini wachawi wanamtumia binadamu huyo kama ndondocha na kuwatumia wanavyotaka, kwa kufanya hivyo jina la Bwana linatukanwa (Zaburi 138:8).

Watu wanaweza kuchukuliwa mateka kwa namna tatu. Kumbuka mtu ni roho anaka kwenye nyumba inaitwa mwili.  Kwakuwa mtu ni roho anaweza kuchukuliwa kwa namna tofauti kuwekwa kifungoni kama ifuatavyo;
1.Anaweza kuchukuliwa mzima kabisa. Wachawi wakimuona mtu anafaa kwenye mambo yao, wanakuja wanafanya uchawi wao kisha wanamchukua kwa kumtoa kwenye mwili wake kisha wanaleta gogo likavaa sura ya mtu huyo. Wakati watu wanahangaika na gogo ili walizike wao wanakuwa wamemchukua mtu huyo kumfanya watakavyo.

Sikumoja Askofu mkuu, Dr. Josephati Gwajima alikwenda msibani mahali, alipokuwa anapita kuaga mwili wa marehemu akaona mgomba umevalishwa suti umewekwa kwenye jeneza, akapita mara ya kwanza na ya pili, akasimama akawambia watu wote walikuwa mahali hapo huyu simtu bali mgomba, wakambishi ndio akasema ‘kwa jina la Yesu’ yule kijana akatoka ndani ya nyumba na kwenye jeneza ukaonekana mgomba kabisa.
Binti huyu alifunguliwa kutoka alikokuwa ametekwa, hakika amewekwa huru kwa jina la Yesu

Jana msavu stendi Morogoro alionekana kijana anaumwa mguu, watu wa stendi wakaamua kuchanga ili kumpeleka hospitali, wakati wanampeleka akatokea mtu anasema jamani mtu huyu si alikufa tanga? Wakamkatalia, lakini walipokwisha mpeleka hospitalini akapotea katika mazingira ya kutatanisha hadi leo hayupo.

Kwa mifano hiyo jifunze kuwa watu wanaweza kuchukuliwa na kufichwa, katika mwili akaonekana amekufa na wakamzika kabisa na kuandika jina lake kwenye msalaba, kumbe mtu huyo amechukuliwa amepelekwa mahali kufanya kazi kichawi. Wanaweza kumchukua mtu na mara nyingine wakamzika kumbe yuko Uganda anafanya kazi benki.

2. Mtu anaweza kuchukuliwa na kupotea kabisa, asife wala asionekane mahali kumbe amechukuliwa kwa namna ya kichawi wakamtowesha kumpeleka sehemu kufanya kazi. Tunajifunza mfano wa Yusufu aliyeuzwa na ndugu zake wakasema kuwa amekufa kumbe wamemuuza misri. Hivyo inawezekana mtu kutoweshwa katika mazingira ya kutatanisha kisha akapelekwa mahali pasipo julikana.

3. Mtu anaweza kuchukuliwa kwa namna ya rohoni. Kwakuwa mtu ni roho wanakuja kiuchawi na kumtoa ndani ya mwili kisha kumpeleka wanako taka (Yohana 6:63). Roho ndiyo itiayo uzima mwili haufai kitu, kwakua mwili bila roho umekufa, wanapochukua roho yake wanapanda roho ya mashetani ndani ya mwili. Ndipo matatizo kadha wa kadha yanamtokea mtu huyo.

Ndiomaana tukimrudisha mtu toka msukuleni anasema nilikuwa Tanga nalima mashamba ya katani, unapo muuliza sasa nani alikuwa kwenye mwili wako? Anasema jini, au paka au mbwa. Unaweza kuona mtu ndani ya familia anasababisha shida, ugomvi kwakuwa si mtu bali ni pepo aliye ndani ya mwili wake.
Mchungaji Dr. Godson Issa akimfungua binti huyu na kumweka huru.

Kuna wakati unaweza kumwona mtu anasumbua kwenye mtaa, mwingine anaacha kazi anatumia fedha vibaya, pia unaweza kuzaa mtoto kwenye familia hatari mno anasumbua sana ukaamua kumchapa kila siku, usimwaribu mtoto huyo kwamaana anaweza kuwa si mtu. Kristo alikuja kuokoa na kurudisha kile kilochotekwa na kuibiwa na leo amekuja ili wewe uokolewe kwa jina la Yesu.

Ulifunga ndoa na mume wako alikuwa safi, mtulivu, mpole lakini gafla anaanza kurudi usiku amelewa, anatoa maneno ya ajabu, unamuuliza umekuwaje? Hana jibu, mtu asiye na maarifa akiona mume wake yuko hivyo anaenda kwa mganga. Usifanye hivyo, mchawi hawezi kukusaidia, acha kwenda kwa mganga wa kienyeji tena mganga wa kienyeji ni mbaya kuliko mchawi, yeye anajua kuweka na kutoa uchawi.  Njoo kwa Yesu, yeye amekuja kuokoa na kurudisha kile kilichopotea, kuna uwezo wako umepotea, kibali chako kimepotea hata huwezi kufuatilia mambo yako, ndoa yako imepotea lakini Kristo amekuja kukuoka wewe kwa jina la Yesu.

Biblia inasema usimwache mwanamke mchawi kuishi (Kutoka 22:18), si kama Mungu alikosea bali ni kwasababu hawa wachawi ni wabaya wanaweza kumchukua mtu, mali yake na uwezo wake wakautumia watakavyo. Siku moja niliwahi kumkuta mtu kwenye kibao cha kanisa, nilipomwoji akawa mkali mno, nikamchukua nikamleta kanisani kisha nikamwombea, baada ya siku mbili mama yake akaja anataka mtoto wake, akasema kuwa alikuwa anapata msaada kupitia mtoto huyo, kumbe walimchukua wanamtumia kichawi. Leo Bwana anataka akutoe kwenye utumwa wa kichawi kwa jina la Yesu.
Showers of Glory Morogoro wakiimba na kucheza mbele za Bwana.

Sababu zinazo sababishwa mtu achukuliwe msukule ni kukosa maarifa, biblia inasema watu wangu wanapotea kwa kukosa maarifa (Hosea4:6), sababu nyingine inasabaibisha mtu kuchukuliwa mateka ni wivu (Matendo 5:17-21), sababu ya tatu ni dhambi. Dhambi inamfanya mwanadamu kukosa ulinzi wa Mungu na kuwa rahisi kwa shetani na mawakala wake kumchukua.
“nikasema, Ee Mungu wangu, nimetahayari, naona haya kuinua uso wangu mbele zako, Mungu wangu; kwa maana maovu yetu ni mengi, hata yamefika juu ya vichwa vyetu, na hatia yetu imeongezeka na kufika mbinguni. Tangu siku za baba zetu tumekuwa na hatia kupita kiasi hata leo; na kwa sababu ya maovu yetu sisi, na wafalme wetu, na makuhani wetu, tumetiwa katika mikono ya wafalme wa nchi hizi, tumepigwa kwa upanga, tumechukuliwa mateka, tumenyang'anywa mali zetu, tumetiwa haya nyuso zetu, kama hivi leo.” (Ezra 9:6-7)

Ili uweze kuwekwa chini ya ulinzi wa Mungu lazima umkiri Yesu kuwa Bwana na mwokozi wa maisha yako, ukisha mpokea Yesu utajifunza maarifa ya Neno la Mungu kwa namna hiyo unakuwa chini ya ulinzi wa Mungu na shetani hawezi kukuchukua mateka wewe kihurahisi, watoto wako na kile ulicho nacho. Mungu akubariki kwa moyo wako uliyo tayari kumfuata Kristo na kuwawaokoa waliotekwa. Ameni.

Share:
Powered by Blogger.

Pages