Sunday, April 29, 2018

KURUDISHWA KUTOKA MASHIMO YA UHARIBIFU



GLORY OF CHRIST TANZANIA CHURCH (GCTC)
KANISA LA UFUFO NA UZIMA MOROGORO
PASTOR DR. GODSON ISSA ZACHARIA

JUMAPILI: 29 APRILI 2018
Mchungaji Dr. Godson Issa Zacharia akifundisha wakati wa Ibada ya leo.

Mashimo ni mahali ambapo pamechimbwa kwa kazi maalum. Yawezekana ikawa shimo kwa ajili ya Kisima au kuhifadhi taka na matumizi mengine. Lakini mashimo haya ni mashimo ya rohoni yanayotumiwa kuleta uharibifu. Mashimo ya uharibifu au, ni mashimo yapo katika ulimwengu wa roho hayaonekani kwa macho ya nyama. Mfalme Daudi anasema alipandishwa kutoka shimo la uharibifu, Mungu alimpandishwa kutoka kwenye shimo la uharibifu. Kupandishwa maana yake alikuwa amenaswa kwenye shimo na alipotoka alikanyaga udongo wa utelezi na Bwana akamsimamisha. Katika mashimo haya watu wengi wametumbukizwa na wamenaswa huko. Katika mashimo haya ni mahali ambako shetani anakaa.

 “Akanipandisha toka shimo la uharibifu, Toka udongo wa utelezi; Akaisimamisha miguu yangu mwambani,  Akaziimarisha hatua zangu.” Zaburi 40:2
 “Malaika wa tano akapiga baragumu, nikaona nyota iliyotoka mbinguni, imeanguka juu ya nchi; naye akapewa ufunguo wa shimo la kuzimu.” Ufunuo wa Yohana 9:1

Ni shimo lililotengenezwa katika ulimwengu wa roho. Shetani alikimbilia katika mashimo ya uharibifu au kuzimu. Mahali pengine mashimo haya yanaitwa mashimo ya kichawi. Mchawi anaweza kutengeneza mashimo ya kukusanya mizukule, au kukusanya mali na kuficha.

Kulikuwa na vita mbinguni; Mikaeli na malaika zake wakapigana na yule joka, yule joka naye akapigana nao pamoja na malaika zake; nao hawakushinda, wala mahali pao hapakuonekana tena mbinguni. Yule joka akatupwa, yule mkubwa, nyoka wa zamani, aitwaye Ibilisi na Shetani, audanganyaye ulimwengu wote; akatupwa hata nchi, na malaika zake wakatupwa pamoja naye. Nikasikia sauti kuu mbinguni, ikisema, Sasa kumekuwa wokovu, na nguvu, na ufalme wa Mungu wetu, na mamlaka ya Kristo wake; kwa maana ametupwa chini mshitaki wa ndugu zetu, yeye awashitakiye mbele za Mungu wetu, mchana na usiku. Nao wakamshinda kwa damu ya MwanaKondoo, na kwa neno la ushuhuda wao; ambao hawakupenda maisha yao hata kufa. Kwa hiyo shangilieni, enyi mbingu, nanyi mkaao humo. Ole wa nchi na bahari! Kwa maana yule Ibilisi ameshuka kwenu mwenye ghadhabu nyingi, akijua ya kuwa ana wakati mchache tu.” Ufunuo 12:7-12

Hapa tunaona kulijuwa na vita mbingu na malaika waliosi wasiotii, walipotaka kupandisha kiti chake juu zaidi ya kile cha Mungu, ndipo kukatokea vita katika ulimwengu wa roho. Joka au Ibilisi alipigana na malaika lakini hakushinda na akatupwa hata nchi. Biblia inasema alitupwa yeye na wale waliokuwa wanashirikiana nao. Biblia inaposema nchi ina maana ni hapa duniani. Hapa duniani angani, bahari na ardhini kuna mashimo ya roho. Mambo yote unayoona katika ulimwengu wa mwili yameanzia katika ulimwengu wa roho. Mfano unapoona meza, kiti au chochote kimeanzia ulimwengu wa roho. Tunakumbuka zamani wafalme walikuwa wanachimba mashimo kuwatesa watu, mashimo yalikuwa na matope.
Baadhi ya Makutano wakimshangilia Bwana baada kuokolewa kutoka nguvu ya mashimo ya uharibifu. 

Shimo hili limetasfiriwa kama kuzimu au ulimwengu wa wafu kwa kiebrania, pia limetasfriwa kama shafti ni shimo ambalo ukiiingia huwezi kupanda. Maana yake yametengenezwa kwa kuchongwa sana. Na mahali pengine limetasfiriwa kama Abis ni shimo lenye giza na taabu sana, kazi au masomo yanakuwa na gizagiza. Shimo lisilokuwa na kimo, yaani ukidumbukia huoni ukifika mwisho. Una kuta mtu anaota unadumbukia lakini hufiki mwisho. Unaona kazi, mume , fedha zinatumbukia lakini leo Bwana atakutoa leo kwa jina Yesu. Mashimo haya ni mabaya sana na kuna watu wengi wametumbukia kwenye haya mashimo.

“Hofu, na shimo, na mtego, vi juu yako, Ee mwenye kukaa duniani.” Isaya 24:17

Kila akaaye dunia anakumbana na hofu, shimo na mitego vipo kwa kila mmoja anayeishi duniani. Mashimo haya wanaanda wachawi, waganga wa kienyeji na mashetani ili kukupeleka shimo.  Wachawi hawakubebi mwili mzima bali wanaweza kuchukua nafsi yako na kupeleka shimonio.

“Lakini utashushwa mpaka kuzimu; Mpaka pande za mwisho za shimo.” Isaya 14:15
 
Kijana huyu anaitwa Peter, hapa alikuwa anatoa ushuhuda namna alivyokuwa akitumikishwa kwenye shimo la uharibifu kule Musoma.
Shimo hili ni refu sana wala huwezi kupanda, mashetani wametengenezwa mashimo na kufanya kama makao makuu. Mizimu inaitwa mizimu kwa sababu ni viumbe vilivyotoka kuzimu. Hii mizimu imewekwa ili ilete uharibifu, hasara, taabu, shida, au kudhoohofisha kazi, afya na ustawi wako. Inawezekana ulishaambiwa wewe hujafanikiwa kwa sababu hujaitumikia mizimu ya babu yako. Unapoweka agano na mizimu ni unakuwa unawasiliana moja kwa moja na viumbe wa kuzimu. Kuzimu linaitwa shimo la uharibifu kwa sababu linavuvia uharibu, kutoka kuzimu.

“Umeniinua nafsi yangu, Ee Bwana, kutoka kuzimu. Umenihuisha na kunitoa Miongoni mwao washukao shimoni.” Zaburi 30:3

Mtu ni roho yenye nafsi inayokaa kwenye mwili. Kuna watu wameibiwa nafsi zao  na kupelekwa kuzimu au shimo.

“Aliyeufanya ulimwengu ukiwa, akaipindua miji yake; Asiyewafungua wafungwa wake waende kwao?” Isaya 14:17

Mtu anapelekwa shimoni na anatumikishwa. Mashetani wanabeba roho yake na mwili wanaweka roho ya joka ya kusumbua watu ili wamtumie. Hii roho inayotolewa inatumiwa kuangusha magari, na katika mwili lile joka linafanya kazi.

“Lakini watu hawa ni watu walioibiwa na kutekwa; wote wamenaswa katika mashimo, wamefichwa katika magereza; wamekuwa mawindo, wala hapana aokoaye; wamekuwa mateka, wala hapana asemaye, Rudisha.” Isaya 42:22
Mungu alimwonyesha Isaya kuna watu wanatenda kazi lakini amechukuliwa wako mashimo, wamefichwa na wamekuwa mawindo, mateka lakini hapana aokoaye. Kumbe mashimo haya ni kwa ajili ya kuficha na kuteka watu.
 
Kijana aliyelala chini anaitwa Daudi alikuwa amelogwa na akawa Kichaa, lakini baada ya kuombewa hapa Ufufuo na Uzima  akawa mzima.  waliosimama ni Mchungaji Kiongozi Dr. Godson Zacharia pamoja na familia ya kijana Daudi wakati akitoa ushuhuda wakati wa Ibada ya leo.
Basi mfalme wa Misri akawaita wale wazalisha na kuwauliza, Kwa nini kufanya jambo hili, na kuwahifadhi watoto waume wawe hai? Wazalisha wakamwambia Farao, Ni kwa sababu hao wanawake wa Kiebrania si kama wanawake wa Kimisri; kwa kuwa ni hodari hao, nao huzaa kabla mzalisha hajapata kuwafikilia. Basi Mungu akawatendea mema wale wazalisha; na hao watu wakaongezeka sana, wakaendelea na kuzidi kuwa na nguvu nyingi. Ilikuwa kwa sababu wale wazalisha walikuwa wakimcha Mungu, akawasimamishia nyumba. Kisha huyo Farao akawaagiza watu wake, akisema, Kila mtoto mwanamume atakayezaliwa mtamtupa mtoni, na kila mtoto mwanamke mtamhifadhi hai.” Kutoka 1:18-22

Mfalme Farao aliona wana wa Izraeli wanaongezeka sana na kwa kasi, basi akaongea na wazalishaji wakiwa wanazalisha kama mtoto wa kiume muueni na wa kike waache waishi. Mashetani wana uwezo wa kuchungulia na kujua kama mtoto huyu akizaliwa atakuwa mkuu, waziri mkuu kumbe kuna mauti imetengenezwa ili mtoto apelekwe shimo. Inawezekana kuna mambo yako yanazaliwa lakini yanakufa haraka haraka, ndoa inaanza, kazi inaanza  zinakufa. Mapepo yanapoona kesho yako unaanza kufanikiwa wanaiua haraka. Wale wazalishaji walikuwa wacha Mungu walikataa kuwaua.

“Maana bila sababu wamenifichia wavu, Bila sababu wameichimbia shimo nafsi yangu.” Zaburi 35:7

Shimo linaweza kuchimbwa na mtu kwa ajili yako au watoto wako. Kuna baadhi ya watu wameshachimbiwa shimo, afya yako imenasa, kukataliwa, shida na huwezi, wamekufichia wavu.

“Amechimba shimo, amelichimba chini sana, Akatumbukia katika handaki aliyoifanya!” Zaburi 7:15
 
Mchungaji akimfungua binti kutoka mashimo ya uharibifu. 
Shimo limechimbwa chini sana, unaona ukianza kujenga nyumba imekwama.

“Mtu asiyefaa kitu huchimba shimo la madhara;  Katika midomo yake mna moto uteketezao.” Mithali 16:27
Mtu asiyefaa kitu ni watu kama wachawi, mganga wa kienyeji, anapanga kukuua wewe. Wewe upo lakini kuna watu wamekuchimbia shimo ili usitoke. Ukiri: Leo natoka kwa jina la Yesu, shimo nililochimbiwa na rafiki, ndugu, bosi wako, au baba nalifukia kwa damu ya mwanakondoo. Mtu anaweza kutengeneza shimo likakaa ndani yako.

“Kinywa cha malaya ni shimo refu;  Anayechukiwa na Bwana atatumbukia ndani yake.” Mithila 22:14

Kinywa cha Malaya ni shimo refu. Kuna binadamu barabarani wanatembea kawaida lakini ni shimo refu na ukiambatana naye unadumbukiwa. Mtu anayefanya uzinzi hawezi kuacha kwa sababu alipofanya kwa mara ya kwanza na hawezi kuacha, mara leo yupo na huyu kesho na yule. Hilo ni shimo limeachia likakumeza. Shimo la uharibifu linaweza kuwa mtu mwenyewe.


“Kwa maana kahaba ni shimo refu; Na malaya ni rima jembamba.” Mithali 23:27

Anayefanya kahaba ni shimo refu, wanakutengenezea ukianza kitu chochote kiharibike.

Kisha mfalme akaenda nyumbani kwake, akakesha usiku kucha, akafunga; na vinanda havikuletwa mbele yake; na usingizi wake ukampaa. Asubuhi mfalme akaondoka mapema, akaenda kwa haraka mpaka penye lile tundu la simba. Naye alipolikaribia lile tundu, akamlilia Danieli kwa sauti ya huzuni; mfalme akanena; akamwambia Danieli, Ee Danieli, mtumishi wa Mungu aliye hai, je! Mungu wako, unayemtumikia daima, aweza kukuponya na simba hawa? Ndipo Danieli akamwambia mfalme, Ee mfalme, uishi milele.” Daniel 6:18-21
 
Showers of Glory Morogoro wakiimba na kucheza mbele za Bwana.
Daniel alitupwa kwenye shimo la Simba, mfalme hakulala na usingizi ulimpaa, mfalme anaweza kukutoa kwenye tundu la samba, yeye anayekuweka ndiyo anayeweza kukutoa. Mfalme hakulala kwa sababbu mtakatifu wa Bwana ametupwa shimoni, Daniel hakuonekana na kosa wala hatia.  Lakini leo tunaye Mfalme Yesu Kristo, ambaye alitoa maisha yake kwa ajili yetu. Yesu halali akiona nyumba, ndoa, kazi ipo shimoni mpaka vyote vimetoka. Mfalme Dario alipoamka asubuhi akamuuliza Daniel Mungu unayemtumikia je amekuokoa? Mungu aliye hai akuokoe na shimo la uharibifu kwa jina la Yesu.

Nao wafanya biashara wa nchi walia na kumwombolezea, kwa sababu hapana mtu anunuaye bidhaa yao tena; bidhaa ya dhahabu, na fedha, na kito chenye thamani, na lulu, na kitani nzuri, na nguo ya rangi ya zambarau, na hariri, na nguo nyekundu; na kila mti wa uudi, na kila chombo cha pembe, na kila chombo cha mti wa thamani nyingi, na cha shaba, na cha chuma, na cha marimari; na mdalasini, na iliki, na uvumba, na marhamu, na ubani, na mvinyo, na mafuta ya mzeituni, na unga mzuri, na ngano, na ng'ombe, na kondoo, na farasi, na magari, na miili na roho za wanadamu.” Ufunuo 18:11-13

Hizi ni bidhaa ambazo wafanyabiashara wa nchi wanazozifanya. Kuna biashara ya miili ya na Roho za wanadamu inaendelea kwenye ulimwengu wa roho. Kumbe mashimo haya ni sehemu ya kutunzia roho za wanadamu waliobiwa. Leo lazima tuwatoe kwa jina la Yesu.

KWA MSAADA ZAIDI NA MAOMBEZI:
FIKA KANISANI,
KANISA LA UFUFUO NA UZIMA MKUNDI MINARA MITATU MOROGORO
AU WASILIANA NASI KUPITIA  
FACEBOOK: Pastor Dr Godson Issa Zacharia
Follow us on INSTAGRAM: pastordrgodson
Follow us on YOUTUBE: Pastor Dr. Godson Zacharia
TEL: +255 719 798 778
BLOG: Ufufuo na Uzima Morogoro

Share:
Powered by Blogger.

Pages