Sunday, February 11, 2018

KUHAMA KUTOKA UFALME WA UHARIBIFU

GLORY OF CHRIST TANZANIA CHURCH (GCTC)

KANISA LA UFUFUO NA UZIMA MOROGORO

SNP DKT. GODSON ISSA ZACHARIA

JUMAPILI: 11 FEBRUARI, 2018

MHUBIRI: MCHUNGAJI, DKT. GODSON ISSA ZACHARIA
Mchungaji Kiongozi, Dkt Godson Issa Zacharia akifundisha maelfu ya makutano katika ibada ya leo.
Duniani kuna falme 2 zinazofanya kazi. Falme hizi 2 zinapingana. Ufalme wa Mungu, huu ni ufalme halali ambao hautikisiki, Ufalme huu ndio watu wanatakiwa kufanya kazi hapa duniani. Ufalme huu ulitoka mbinguni na kuletwa duniani.

“Akawaambia, Msalipo, semeni, Baba [yetu uliye mbinguni], Jina lako litakaswe, Ufalme wako uje, [Mapenzi yako yatimizwe, hapa duniani kama huko mbinguni.]” Luka11:2
Hapa Yesu alikuwa anawafundisha wanafunzi wake namna ya kusali. Aliwaambia kwamba Baba yetu yupo mbinguni, jina lako litakaswe, ufalme wako  uje, na mapenzi yako yatimizwe hapa duniani kama huko mbinguni. Ufalme uliombwa kutoka mbinguni na ukaja kutoka mbinguni.
Hapa duniani tunapoishi uraia wetu si hapa bali ni mbinguni ni kwa sababu mtu ni roho na anakaa kwenye nyumba ambayo ni mwili na alipuliziwa pumzi kutoka mbinguni. Mfano wamarekani wana ufalme wao wakitaka kuja Tanzania wanatengeneza ubalozi.
“Basi kwa kuwa tunapokea ufalme usioweza kutetemeshwa, na mwe na neema, ambayo kwa hiyo tumtolee Mungu ibada ya kumpendeza, pamoja na unyenyekevu na kicho;” Waebrania 12:28
Ufalme wa Mungu hautetemeshwi.
Kuna ufalme wa uharibifu/na ufalme wa shetani, ufalme huu ni batili (hauna kibali) ni mtu aliyejiapisha mwenyewe,  ni ufalme ambao haujaruhusiwa na aliyeumba mbingu na nchi. Ni ufalme unaofanya kazi hapa duniani.
Kila ufalme unaye mfalme.
Platform Ministry wakiongoza sifa katika ibada ya leo.
“Mwivi haji ila aibe na kuchinja na kuharibu; mimi nalikuja ili wawe na uzima, kisha wawe nao tele.” Yohana 10:10
Hapa tunajifunza mfalme wa uharibifu kwamba ni mwivi haji ila aibe na kuchinja na kuharibu. Ila Yesu alikuja ili tuwe na uzima huyu ni mfalme wa ufalme wa mbinguni.
“Na juu yao wanaye mfalme, naye ni malaika wa kuzimu, jina lake kwa Kiebrania ni Abadoni, na kwa Kiyunani analo jina lake Apolioni.” Ufunuo wa Yohana 9:11
Biblia inasemaa yupo mfalme ambaye ni Ibilisi kwa Kiebrania ni Abadoni, na kwa Kiyunani analo jina lake Apolioni au muharabu.
“Sisi tunajua ya kuwa tumepita toka mautini kuingia uzimani, kwa maana twawapenda ndugu. Yeye asiyependa, akaa katika mauti.” 1 Yohana3:14
Sisi tukiamini tumepita toka mautini na kuingia uzimani. Kuna ufalme unatawala mautini.
Ukiri: Kwa jina la Yesu, ingawa nina maumivu makali najua ya kwamba nimepita toka mautini na kuingia uzimani.
“Amin, amin, nawaambia, Yeye alisikiaye neno langu na kumwamini yeye aliyenipeleka yuna uzima wa milele; wala haingii hukumuni, bali amepita kutoka mautini kuingia uzimani.” Yohana 5:24
Kuna watu wapo duniani wanatembea lakini wameshakufa, lakini Biblia inasema yeyote atakayeamini yu na uzima tele na amepita kutoka mautini na kuingia uzimani. Biblia inasema tumekuwa wafu ni kwa sababu ya makosa na dhambi zetu. Ili uvuke kutoka mautini na kuingia uzimani  ni lazima uvuke kwa kumwamini Yesu.
Mfalme wa uharibifu ni kama mvuvi haramu, Mfalme huyu wa uharibifu amevua vitu vingi sana, amevua mimba, watoto, kazi, ndoa, amevua watu na kuwaweka msukuleni amewaweka mashimoni.
“Kulikuwa na vita mbinguni; Mikaeli na malaika zake wakapigana na yule joka, yule joka naye akapigana nao pamoja na malaika zake; nao hawakushinda, wala mahali pao hapakuonekana tena mbinguni. Yule joka akatupwa, yule mkubwa, nyoka wa zamani, aitwaye Ibilisi na Shetani, audanganyaye ulimwengu wote; akatupwa hata nchi, na malaika zake wakatupwa pamoja naye.” Ufunuo 12:7-9
Mfalme wa uharibifu amevuna vitu vingi sana,

“Jinsi ulivyoanguka kutoka mbinguni, Ewe nyota ya alfajiri, mwana wa asubuhi! Jinsi ulivyokatwa kabisa, Ewe uliyewaangusha mataifa! Nawe ulisema moyoni mwako, Nitapanda mpaka mbinguni, Nitakiinua kiti changu juu kuliko nyota za Mungu; Nami nitaketi juu ya mlima wa mkutano,  Katika pande za mwisho za kaskazini. Nitapaa kupita vimo vya mawingu, Nitafanana na yeye Aliye juu.  Lakini utashushwa mpaka kuzimu; Mpaka pande za mwisho za shimo. Wao wakuonao watakukazia macho, Watakuangalia sana, wakisema, Je! Huyu ndiye aliyeitetemesha dunia, Huyu ndiye aliyetikisa falme; Aliyeufanya ulimwengu ukiwa, akaipindua miji yake; Asiyewafungua wafungwa wake waende kwao?” Isaya 14:12-17
Maelfu ya makutano wakisikiliza somo la leo la kuhama kutoka ufalme wa uharibifu.
Mfalme huyu ameangusha mataifa, mfalme huyu anatakiwa apigwe, amepanga shida,matatizo, lazima tumpige na arudi kuzimu. Ufalme wa uharibifu una makao makuu matatu, Baharini, nchi kavu na angani. Ufalme huu wa uharibifu una gereza au shimo na kuzimu.
“Lakini watu hawa ni watu walioibiwa na kutekwa; wote wamenaswa katika mashimo, wamefichwa katika magereza; wamekuwa mawindo, wala hapana aokoaye; wamekuwa mateka, wala hapana asemaye, Rudisha.” Isaya 42:22
Watu wametekwa waishi kule wanalishwa nyama za watu,  wana kunywa damu za watu. Ufalme huu wa uharibifu unaandaa mpango kazi ambao utachagua nani aoe/kuolewa, nani atapata kazi. Kwenye ufalme huu kuna uchawi, wizi, na anachinja na kutengeneza mizoga.
“Ole wake mji wa damu! Umejaa mambo ya uongo na unyang'anyi; mateka hayaondoki. Kelele za mjeledi, kelele za magurudumu yafanyayo kishindo; na farasi wenye kupara-para, na magari ya vita yenye kuruka-ruka; mpanda farasi akipanda, na upanga ukimeta-meta, na mkuki ukimemetuka; na wingi wa waliouawa, na chungu kubwa ya mizoga; mizoga haina mwisho; wanajikwaa juu ya mizoga yao. Kwa sababu ya wingi wa ukahaba wa yule kahaba mzuri, yule bibi wa mambo ya uchawi, auzaye mataifa kwa ukahaba wake, na jamaa za watu kwa uchawi wake.” Nahumu 3:1-4
Japokuwa umetekwa, Bwana akusimamishe tena. Ufalme wa uharibifu umejaa hila, na wasaidizi wake ni mashetani, majoka.
“hata mfalme mwingine akainuka juu ya Misri, asiyemfahamu Yusufu. Huyo akawafanyia hila kabila yetu, na kuwatenda mabaya baba zetu, akiwaamuru wawatupe watoto wao wachanga, ili wasiishi.” Matendo 7:18-19
Unakuta mtu anajifungua mtoto anaambiwa ameshakufa, au amezaliwa baada ya mwezi anakuwa na degedege. Hizi ni hila za mfalme wa uharibifu. Mfalme huyu wa uharibifu ni muuaji.
Children Ministry wakiimba na kucheza katika ibada ya leo.
“Ninyi ni wa baba yenu, Ibilisi, na tamaa za baba yenu ndizo mpendazo kuzitenda. Yeye alikuwa mwuaji tangu mwanzo; wala hakusimama katika kweli, kwa kuwa hamna hiyo kweli ndani yake. Asemapo uongo, husema yaliyo yake mwenyewe; kwa sababu yeye ni mwongo, na baba wa huo.” Yohana 8:44
Kwenye ufalme wa uharibifu mipango yao ni kuchinja, kuua ,a kuharibu. Na hata wachawi wakikutana mahali mipango yao ni kuua, kuchinja na kuharibu.  Yamkini umeibiwa furaha yako haipo, kumbe yupo muharibifu amepanga ili uibiwe, lakini leo kwa jina la Yesu Kristo yeye alikuja ili tuwe na uzima tele, leo namfuata kwa jina la Yesu  namkamata nakukanyaga kwa jina la Yesu achia kwa jina la Yesu.
Kila kitu kinachotokea kwenye ulimwengu wa mwili kinaanzia katika ulimwengu wa roho hapahapa duniani. Ufalme wa uharibifu unaiba akili.
Wakazi wa ufalme wa uharibifu.
1.     Wakazi wa ufalme huu wana magonjwa mengi ambayo hayaponi, ni kwa sababu mkuu wa ufalme anapanda magonjwa.
2.     Wakazi wa ufalme huu wamejawa na tabu, tabu imekuwa kama makazi yako.
3.     Umasikini; wakazi wa ufalme huu wamejawa umaskini, unaweza kumkuta mtu ameokoka lakini ni masikini.
4.     Majuto; wakazi wa ufalme huu wana majuto mengi, unakuta mtu anasema najuta kuzaa watoto, hii ni kwa sababu unaishi kwenye ufalme wa uharibifu.
5.     Kukataliwa & Mikosi; wakazi wa ufalme huu wamejaa mikosi na kukataliwa.
6.     Msukule, kuibiwa, mauti; wakazi wa ufalme huu wamejawa na kuchukuliwa msukule, wanaibiwa ndoa, kazi, mchumba, safari. Pia wamejawa na vifo, vifo vya kazi.
7.     Huzuni; wakazi wa ufalme huu wamejawa na huzuni.Lakini Yesu alikuja ili kutuondolea huzuni.
Muumini akifunguliwa kutoka kwenye ufalme wa uharibifu.

8.      Chuki; wakazi wa ufalme wamejaa chuki sana.
WAKAZI WA UFALME WA MUNGU
Huu ni ufalme halisi ambao Bwana aliuleta kutoka mbinguni. Bwana aliutengeneza kama ubalozi ili ukae kwetu. Mimi na wewe tumeumbwa kutoka kwenye ufalme wa Mungu ambao hautikisiki.
Ufalme huu wa Mungu huwa unakuja kwetu na kuupokea, kwa kuwa tunapokea ufalme huu tumtolee Bwana ibada ya kutengeneza. Kwenye ufalme huu kuna uzima. Yohana 10:10
“Bali ninyi mmeufikilia mlima Sayuni, na mji wa Mungu aliye hai, Yerusalemu wa mbinguni, na majeshi ya malaika elfu nyingi, mkutano mkuu na kanisa la wazaliwa wa kwanza walioandikwa mbinguni, na Mungu mwamuzi wa watu wote, na roho za watu wenye haki waliokamilika,  na Yesu mjumbe wa agano jipya, na damu ya kunyunyizwa, inenayo mema kuliko ile ya Habili.” Waebrania 12:22-24
Hawa ni wakazi wa ufalme wa Mungu, Mungu Baba mwenyewe, majeshi ya malaika elfu nyingi, kanisa la wazaliwa wa kwanza, Mungu mwamuzi wa watu wote, roho za watu wenye haki, Yesu Kristo, na damu inayonena mema.
Kwenye ufalme huu hakutakiwi magonjwa kwa sababu ipo damu inayonena mema. Magonjwa haya ni mapando ya ufalme wa uharibifu
“Maana moyo wake hapendi kuwatesa wanadamu. Wala kuwahuzunishaMaombelezo 3:33
Hapa Mungu hapendi kuwahuzunisha watu, huzuni ni pando la ufalme wa uharibifu. Kwenye ufalme huu hakuna mikosi. Mungu wakati anatuumba alituwekea uwezo wa kumiliki na kutawala mipango hii iliwekwa kabla ya kuzaliwa. Kuishi, kufanikiwa, kuoa/kuolewa, utamiliki na kutiisha.
“Kabla sijakuumba katika tumbo nalikujua, na kabla hujatoka tumboni, nalikutakasa; nimekuweka kuwa nabii wa mataifa.” Yeremia 1:5
Ufalme huu unapanga mipaka.
Mamia ya waumini waliompokea Yesu Kristo kuwa Bwana na Mwokozi wa maisha yao katika ibada ya leo.
“Bwana akamwambia Abramu, Toka wewe katika nchi yako, na jamaa zako, na nyumba ya baba yako, uende mpaka nchi nitakayokuonyesha; nami nitakufanya wewe kuwa taifa kubwa, na kukubariki, na kulikuza jina lako; nawe uwe baraka; nami nitawabariki wakubarikio, naye akulaaniye nitamlaani; na katika wewe jamaa zote za dunia watabarikiwa.”Mwanzo 12:1-3

Hapa Mungu anakupa mipaka ya kumiliki, pia atakufanya uwe taifa kubwa.
“Angalieni, nawawekea mbele yenu hivi leo baraka na laana;”Torati 11:26
Hapa Mungu anasema ukiyashika maagizo yake ameweka Baraka mbele yako.
“Maana mmejua neema ya Bwana wetu Yesu Kristo, jinsi alivyokuwa maskini kwa ajili yenu, ingawa alikuwa tajiri, ili kwamba ninyi mpate kuwa matajiri kwa umaskini wake.” 2 Wakorintho 8:9
Yesu alifanyika kuwa masikini ili mimi na wewe tuwe matajiri, ukiona wewe si tajiri ujue unaishi kwenye ufalme wa uharibifu.
“ili kwamba baraka ya Ibrahimu iwafikilie Mataifa katika Yesu Kristo, tupate kupokea ahadi ya Roho kwa njia ya imani.” Wagalathia 3:14
Ibrahim kama baba yetu  alikuwa na mali nyingi, na sisi yatupasa kumiliki na kuwa tajiri kama Baba yetu wa Imani.
Inawezekana umeokoka na unatakiwa uishi kwenye ufalme wa Mungu, lakini wakakuzunguka na wakakuweka katika ubalozi wa kishetani.
“Nao waimba wimbo mpya wakisema, Wastahili wewe kukitwaa hicho kitabu na kuzifungua muhuri zake; kwa kuwa ulichinjwa, ukamnunulia Mungu kwa damu yako watu wa kila kabila na lugha na jamaa na taifa, ukawafanya kuwa ufalme na makuhani kwa Mungu wetu; nao wanamiliki juu ya nchi.Ufunuo 5:9-10
“Bali ninyi ni mzao mteule, ukuhani wa kifalme, taifa takatifu, watu wa milki ya Mungu, mpate kuzitangaza fadhili zake yeye aliyewaita mtoke gizani mkaingie katika nuru yake ya ajabu;1 Petro 2:9
Shetani anaitwa mungu wa dunia hii, lakini Mungu aliamua kushusha ubalozi wake ndani yangu na ndani yako. Lakini wakakuiba na kuwekwa kwenye ufalme wa uharibifu.
KWA MSAADA ZAIDI NA MAOMBEZI WASILIANA NASI KUPITIA
FACEBOOK: Pastor Dr Godson Issa Zacharia
Follow us on INSTAGRAM: pastordrgodson
Follow us on YOUTUBE: Pastor Dr.Godson Zacharia
TEL: +255 719 798 778
(WhatsAssp & SMS only)
BLOG: Ufufuo na Uzima Morogoro       http://ufufuonauzimamorogoro.blogspot.com/



Share:
Powered by Blogger.

Pages