Sunday, February 4, 2018

MASHUJAA WA UFALME

GLORY OF CHRIST TANZANIA CHURCH (GCTC)

KANISA LA UFUFUO NA UZIMA MOROGORO

SNP  DKT. GODSON ISSA ZACHARIA

JUMAPIL: 4 FEBRUARI, 2018

MHUBIRI: MCHUNGAJI, DKT. GODSON ISSA ZACHARIA

Mchungaji Dkt. Godson Issa Zacharia akifundisha kuhusu Mashujaa wa Ufalme
“Basi hawa ndio wakuu wa mashujaa aliokuwa nao Daudi, waliojitia nguvu pamoja naye katika ufalme wake, pamoja na Israeli wote, ili kumfanya awe mfalme, sawasawa na neno la Bwana alilonena juu ya Israeli.” 1 Mambo ya Nyakati 11:10

Shujaa ni mtu jasiri, asiyeogopa chochote, ni mtu ambaye yuko tayari kutetea haki yake au kile kitu anachokiamini. Ni mtu ambaye hawezi kunyamza mpaka kile anachoomba kitokee kwenye maisha yake. Ni mtu anayejiamaini na ana udhubutu yeye mwenyewe ili kuleta ushindi katika nyumba yake au kanisani. Ni mtu mwenye uwezo wa kukabili na kuvumilia dhiki ili kufika kwenye mafanikio yake.

Shujaa wa ufalme ni mtu ambaye ni jasiri kuelekea  nchi ya ahadi ili amiliki ahadi ya nchi kama Mungu alivyoagiza. Kuwa shujaa wa ufalme ni agizo la Bwana. Kwenye ufalme wa mwanakondoo kuna mashujaa wanatakiwa watengenezwe. Mungu alimuagiza Joshua kuwa shujaa na moyo wa uhodari.
           Baadhi ya Makutano wakisikiliza kwa umakini kuhusu Mashujaa wqa Ufalme.

Uwe hodari na moyo wa ushujaa, maana ni wewe utakayewarithisha watu hawa nchi hii niliyowaapia baba zao ya kwamba nitawapa. Uwe hodari tu na ushujaa mwingi, uangalie kutenda sawasawa na sheria yote aliyokuamuru Musa mtumishi wangu; usiiache, kwenda mkono wa kuume, au wa kushoto, upate kufanikiwa sana kila uendako. Kitabu hiki cha torati kisiondoke kinywani mwako, bali yatafakari maneno yake mchana na usiku, upate kuangalia kutenda sawasawa na maneno yote yaliyoandikwa humo; maana ndipo utakapoifanikisha njia yako, kisha ndipo utakapositawi sana. Je! Si mimi niliyekuamuru? Uwe hodari na moyo wa ushujaa; usiogope wala usifadhaike; kwa kuwa Bwana, Mungu wako, yu pamoja nawe kila uendako” Yoshua 1:6-9.

Joshua aliambiwa awe hodari na moyo wenye ushujaa. Watu wote ambao ni hodari wana moyo wa ushujaa. Mungu anataka ufanikiwe, upate mali, usome ili upate haya ni lazima ushike sheria yake katika njia iliyonyooka. Kupata moyo wa shujaa ni lazima kuondoa woga. Kuwa shujaa katika nchi ni agizo la Bwana.

“Vaeni silaha zote za Mungu, mpate kuweza kuzipinga hila za Shetani.” Waefeso 6:11

Ushujaa hauji kwa sababu ya ukoo uliotokea, au umesoma sana, au una fedha nyingi. Ili uwe shujaa na hodari unahitaji uwezo na nguvu kutoka kwa Bwana kwa   kuvaa silaha zote za Mungu. Kumbuka Moyo wa ushujaa ni agizo la Bwana. Moyo wa ushujaa unapokelewa, huu moyo kuna sehemu upo. Unapokuwa na jambo la kufanya Bwana anakupa moyo wa shujaa.
Platform team wakiongoza kipindi cha sifa na kuabudu katika ibada ya leo.

“Wewe u rungu langu na silaha zangu za vita; kwa wewe nitawavunjavunja mataifa; na kwa wewe nitaharibu falme;” Yeremia 51:20
Wewe ni rungu na silaha za Bwana, kila unapokwenda uende kama silaha, wewe ni upanga, moto, kifaru, wewe ni kisu cha Bwana. Kinachokupa wasiswasi ni kwa sababu hujajua wewe ni nani. Leo ujue kwamba wewe ni shujaa. Duniani kuna matatizo mengi lakini yanahitaji apatikane mtu ambaye ni shujaa.
“Basi Daudi akaondoka huko, akakimbilia pango la Adulamu; na ndugu zake na watu wote wa mbari ya baba yake waliposikia habari hiyo, wakamwendea huko. Na kila mtu aliyekuwa katika hali ya dhiki, na kila mtu aliyekuwa na deni, na watu wote wenye uchungu mioyoni mwao, wakakusanyika kwake; naye akawa jemadari wao; nao waliokuwa pamoja naye walipata kama watu mia nne.” 1 Samweli 22:1-2
Daudi alikuwa ni mtu kabisa lakini ndani yake aliwekewa moyo wa ushujaa na moyo wa kusaidia. Daudi alikuwa na moyo wa kuwasaidia  watu waliofungwa. Daudi alimuua Goliath, wanawake wakatunga wimbo, ambao ulikuwa ulikuwaunasema Sauli ameua maelfu lakini Daudi ameua makumi elfu. Roho ya wivu ikamwingia Sauli na akaanza kumwinda Daudi kwa ajili ya ule moyo wa ushujaa aliokuwa nao, Daudi akakimbilia pangoni. Kwa kuwa alikuwa na moyo wa ushujaa watu walimfuata Daudi pangoni. Watu hawa walijua Daudi anao uwezo wa kuwaondolea madeni, uchungu, na kuachwa na watu. Daudi alifanyika kuwa jemerdari (kiongozi) wa watu hao. Jemedari kwa kingereza ni ‘Captain’, hii ni nafasi ya juu katika nafasi za uongozi jeshini. Kuna watu wakipata shida wanakimbilia kwa mganga wa kienyeji, au mchawi, ndugu lakini wewe mkimbilie Daudi wako wa leo. Kuna mtu ambaye Mungu amemweka ili akusaidie wewe.
Katika ulimwengu wa leo watu wanapenda watu wenye mafanikio ila ni mashujaa peke yao wanaweza kukaa na watu wenye dhiki. Watu hawa wakishafanikiwa wataambatana na Daudi.


“Haya ndiyo majina ya mashujaa aliokuwa nao Daudi; Yashobeamu  Mhakmoni, mkuu wa maakida; huyo aliliinua shoka lake juu ya watu mia nane waliouawa pamoja. Na baada yake kulikuwa na Eleazari, mwana wa Dodai, Mwahohi, mmojawapo wa wale mashujaa watatu waliokuwa pamoja na Daudi; walipowatukana Wafilisti waliokuwa wamekusanyika huko ili kupigana, na watu wa Israeli walikuwa wamekwenda zao; huyo aliinuka, akawapiga Wafilisti hata mkono wake ukachoka, na mkono wake ukaambatana na upanga; naye Bwana akafanya wokovu mkuu siku ile; nao watu wakarudi nyuma yake ili kuteka nyara tu. Na baada yake kulikuwa na Shama, mwana wa Agee, Mharari; nao Wafilisti walikuwa wamekusanyika huko Lehi, palipokuwapo konde lililojaa midengu; nao watu wakawakimbia Wafilisti; ila huyo alisimama katikati ya konde lile, akalipigania, akawaua Wafilisti; naye Bwana akafanya wokovu mkuu. Tena, watatu miongoni mwa wale thelathini waliokuwa wakuu wakashuka, wakamwendea Daudi wakati wa mavuno mpaka pango la Adulamu, na kikosi cha Wafilisti walikuwa wamefanya kambi katika bonde la Warefai. Naye Daudi wakati ule alikuwako ngomeni, na jeshi la Wafilisti wakati ule walikuwako Bethlehemu.” 2 Samweli 23:8-14

Children ministry wakicheza na kumsifu Mungu katika ibada ya leo.
“Tena, Abishai, nduguye Yoabu, mwana wa Seruya, alikuwa mkuu wa wale watatu. Huyo aliuinua mkuki wake juu ya watu mia tatu, akawaua, akawa na jina kati ya wale watatu. Tena Benaya, mwana wa Yehoyada, mtu hodari wa Kabseeli aliyekuwa amefanya mambo makuu; aliwaua simba wakali wawili wa Moabu, k pia akashuka akamwua simba katikati ya shimo wakati wa theluji; huyo naye akamwua Mmisri, mtu mrefu; naye huyo Mmisri alikuwa na mkuki mkononi; lakini yeye alimshukia na gongo, akamnyakulia Mmisri mkuki mkononi mwake, akamwua kwa mkuki wake mwenyewe. Hayo ndiyo aliyoyafanya Benaya, mwana wa Yehoyada, akawa na jina kati ya wale mashujaa watatu.” 2 Samweli 18, 20-22
Daudi alikuwa mfalme kwa muda mrefu ni kwa sababu alisimama na watu wenye dhiki na shida na watu wale walikuwa mashujaa wa Daudi. Kama una dhiki ya ndoa, ya watoto, kazi, biashara leo Bwana atakutoa kwenye dhiki hiyo. Bwana anataka uwe shujaa wa ufalme.

Yesu akasema njooni kwangu nyie wasumbukao na wenye kulemewa na mizigo. Hii ni tabia ya Ufalme wa watu wa mbinguni. Ilikuwa tabia ya Daudi kuwaonea huruma wale walioonewa na wenye uchungu. Hata sasa Yesu anawaita na amekusadia kuwafundisha na kuwabadilisha ili wawe mashujaa wa ufalme. Omba, pambana na shindana na falme za giza ili umiliki Baraka zako katika ulimwengu wa roho na hatimaye utastawi kwa jina la Yesu.
 “Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami 0nitawapumzisha.” Mathayo 11:28
Shujaa wa Bwana akifunguliwa kutoka kwenye vifungo.
KWA MSAADA ZAIDI NA MAOMBEZI WASILIANA NASI KUPITIA
FACEBOOK: Pastor Dr Godson Issa Zacharia
Follow us on INSTAGRAM: pastordrgodson
Follow us on YOUTUBE: Pastor Dr.Godson Zacharia
TEL: +255 719 798 778
(WhatsAssp & SMS only)
BLOG: Ufufuo na Uzima Morogoro       http://ufufuonauzimamorogoro.blogspot.com/



Share:
Powered by Blogger.

Pages