JUMAPILI: 08 NOVEMBER 2015 –
UFUFUO
NA UZIMA MOROGORO
Na:
STEVEN NAMPUNJU (RP)
& DR. GODSON ISSA ZACHARIA (SNP)
Utangulizi
wa Somo: Nyota nini? Nyota ni kiashiria cha rohoni kinachoonesha
mtu atakuwa nini au hatima yake baadae. Hatima na matukio ya baadae au mwisho
wa maisha ya mtu ndiyo ambavyo huitwa ‘nyota ya mtu’. Mafanikio ya mtu
hayatokani na elimu aliyo nayo, au mali zake bali hutokana na nyota yake. Hata
hivyo, hivi viashiria vya mtu kuwa atakuwa nani baadae huweza kuibiwa. Mamajusi
pamoja na kwamba watoto waliozaliwa walikuwa wengi kipindi kile, lakini wao walienda
moja kwa moja kwa mtoto Yesu, kwa sababu ya nyota aliyokuwa nayo ya kuwa “mfalme”.
Mambo yahusuyo nyota yanatufundisha kuwa:
1. Kila mtu anayo nyota: tena nyota hiyo hutoa tafsiri
2. Nyota huweza kuonekana:
Ndiyo maana mamajusi walisafiri mwendo mrefu kuifuatilia hii nyota. Kumbe nyota
ya mtu yaweza kusababisha safari
zitengenezwe. Endapo kwako hayupo mtu anayekuja kutembelea nyumbani kwako ni kwa sababu
nyota yako haijaonekana. Siri kubwa watakapoiona nyota basi wasiokuwa wageni
kwako watakuja kwako, tena wakiwa na zawadi
mikononi mwao. Nyota yako ikionekana watakaokuja kwako hakuna hata haja ya
kuwaambia walete nini, kwani watabeba fedha na zawadi kwa ajili yako. Watatokea
mbali, wengine China, Japan n.k watakuja kwako.
3. Nyota yaweza kufuatwa:
Wale Mamjusi walitokea mbali ili kuifuata nyota
4. Nyota ikionekana huleta zawadi /
utajiri: Chanzo kikubwa cha
kufanya hawa mamajusi waje si tu kuiona
nyota, bali kuleta na zawadi. Ukiwa na nyota utapata vyote unavyohitaji.
MHUBIRI
9:11…[Nikarudi, na kuona chini ya jua,
ya kwamba si wenye mbio washindao katika michezo, wala si walio hodari
washindao vitani, wala si wenye hekima wapatao chakula, wala si watu wa ufahamu
wapatao mali, wala wenye ustadi wapatao upendeleo; lakini wakati na bahati
huwapata wote.]….Wakati ukifika na bahati nayo hufika. Ili upate itategemea na wakati wako. Upo wakati ukifika mtu fulani
anapaswa kuwa nani‼ Ili ufanikiwe
unahitaji wakati. Mamajusi wao waliuona wakati wa Yesu kwamba huyu anayezaliwa ni "Mfalme wa Wayahudi". Mamajusi
waliweza kuyaona haya hata kabla ya watu waliopo karibu na ukoo wa Yesu kuyajua. Ni maombi yetu leo kuwa ‘watu wajifunze kujua wakati’.
Baadhi ya wazazi hujisahau na kutabiria watoto wao mabaya: Mfano: wazazi
wanaosema “nimezaa huyu binti
kahaba” / nimempata huyu kijana wa kiume jambazi”
Mungu ameviweka vipawa ndani ya maisha ya watu. Wapo
watu ambao mafanikio yao huja kwa njia ya kusoma, wengine Mungu amewawekea
vipawa vya biashara ili kupitia hivyo wafanikiwe. Lakini pia wapo
wanaolazimisha kutumia nyota zisizokuwa zao, na mara nyingi hutumia nguvu za
giza. Leo kataa nyota yako kutumiwa na watu wengine kwa Jina la Yesu
MIFANO
YA WATU NA NYOTA ZAO KATIKA BIBLIA
1. Musa:
Mungu anataka Musa akawatoe Israeli wote kutokaMisri. Hata hivyo Musa
akajitetea kuwa siyo msemaji, kama ilivyoandikwa katika KUTOKA 4:10…[Musa akamwambia Bwana Ee Bwana, mimi si msemaji, tokea zamani, wala
tokea hapo uliposema na mtumishi wako; maana mimi si mwepesi wa kusema, na
ulimi wangu ni mzito.]… Musa hivyo aliteuliwa
kama kiongoozi msikilizaji wa sauti ya Mungu. Musa hata hivyo hakujua
kuwa anayo nyota / kipawa cha uongozi.
2. Haruni:
Huyu aliteuliwa na Mungu kama msemaji. KUTOKA
4:11-14…[Bwana akamwambia,
Ni nani aliyekifanya kinywa cha mwanadamu? Au ni nani afanyaye mtu kuwa bubu au
kiziwi, au mwenye kuona, au kuwa kipofu? Si mimi, Bwana? 12 Basi sasa, enenda,
nami nitakuwa pamoja na kinywa chako, na kukufundisha utakalolinena. 13
Akasema, Ee Bwana, nakuomba, tuma kwa mkono wake huyo utakayemtuma. 14 Hasira
ya Bwana ikawaka juu ya Musa, akasema, Je! Hayuko Haruni, ndugu yako, Mlawi?
Najua ya kuwa yeye aweza kusema vizuri. Pamoja na hayo, tazama, anakuja kukulaki;
naye atakapokuona, atafurahi moyoni mwake.]…Mungu anamkemea
Musa, kumwambia kuwa Haruni ameteuliwa kuwa msemaji mkuu. Mungu alitaka Musa awe Mungu kwa
Haruni. Haruni ni mzuri katika kushawishi. Imeandikwa katika KUTOKA 7:7..[Huyo Musa alikuwa ni mtu wa miaka
themanini umri wake, na Haruni alikuwa ni mtu wa miaka themanini na mitatu,
hapo waliponena na Farao.].. Kwa upande wa umri, Haruni (83) ni mzee
zaidi ya Musa (80), lakini yeye ndiye
zaidi mahiri wa kuongea.
WALIOPEWA
NYOTA NA MUNGU KATIKA BIBLIA
1. Watu
wenye hakima na uwezo. Imeandikwa katika
ZABURI 45:2…[Wewe u mzuri sana kuliko wanadamu; Neema imemiminiwa
midomoni mwako, Kwa hiyo Mungu amekubariki hata milele.]
2. Watu
wenye roho ya wepesi. Ukiwa na roho ya
uziot Mungu hakupatii nyota. ZABURI 51:2…[Unioshe kabisa na uovu wangu, Unitakase dhambi zangu.3
Maana nimejua mimi makosa yangu Na dhambi yangu i mbele yangu daima.]…Mtu
aliye tayari kuyakubali makosa yake. Siyo kama Adamu alivyoulizwa na Mungu
akasema ‘siyomimi ila yulemwanamke uliyenipa’. Mungu anaweka nyota kwa watu wa
aina hii kwa sababu wapotayari. Wapo pia watu
wenye mioyo mizito: MITAHALI
25:20…[Amwimbiaye nyimbo
mtu mwenye moyo mzito, Ni kama yeye avuaye nguo wakati wa baridi; Ni kama siki juu ya magadi.]….Moyo
mzito hautakiwi hata kidogo.
Imeandikwa pia katika KUTOKA 8:15…[Lakini Farao alipoona ya kuwa pana nafuu, akaufanya moyo
wake kuwa mzito, asiwasikize; kama Bwana alivyonena.]…Mwenye
moyo mzito hutamani shida iishe lakini baada ya nafuu huufanya moyo wake kurudia kuwa mzito, kama Farao alivyofanya.
Kutokana na moyo mzito, Farao na watu wake walipatwa na msiba wa watoto wao na
mifugo yao.
KUNA
HAJA GANI YA KUIRUDISHA NYOTA
ILIYOIBIWA?
1. Nyota ikionekana huwa na furaha
kubwa: Wapo watu leo hii ambao hawana furaha kwa sababu ya nyota kutoonekana
kwapo. MATHAYO 2:10…[ Nao walipoiona ile nyota, walifurahi furaha kubwa mno.]….Yaani
pale nyota ilipopotea wale mamajusi hawakuwa na furaha tena. Mamajusi walikuwa
wakijiuliza kwamba zawadi walizozibeba
watazipeleka wapi?
Wapo ambao nyota zao
zimepotea na wale waliobeba zawadi kwa
ajili yao hawana furaha. Wapo walioahidiwa kuchumbiwa aukuolewa lakini mara nyota zao zilipopotea
furaha zao zikabakia kuwa majuto. Nyota ikirudi,furaha inarudi. Nyota ikirudi
amani inarudi
2. Nyota ya mtu inaweza kubadilisha
historia ya mji: Mahali pale ambapo palidharauliwa
heshima itatokea. MATHAYO 2:1-6..[ Yesu alipozaliwa katika
Bethlehemu ya Uyahudi zamani za mfalme Herode, tazama, mamajusi wa mashariki
walifika Yerusalemu, wakisema, 2 Yuko wapi yeye aliyezaliwa mfalme wa Wayahudi?
Kwa maana tuliiona nyota yake mashariki, nasi tumekuja kumsujudia. 3 Basi
mfalme Herode aliposikia hayo, alifadhaika, na Yerusalemu pia pamoja naye. 4
Akakusanya wakuu wa makuhani wote na waandishi wa watu, akatafuta habari kwao,
Kristo azaliwa wapi? 5 Nao wakamwambia, Katika Bethlehemu ya Uyahudi; kwa maana
ndivyo ilivyoandikwa na nabii, 6 Nawe Bethlehemu, katika nchi ya Yuda, Hu mdogo
kamwe katika majumbe wa Yuda; Kwa kuwa kwako atatoka mtawala Atakayewachunga
watu wangu Israeli.]…Kilichowapeleka mamajusi Yerusalem ni ile
nyota ya Yesu, na kwa kuwa mji huu
ulikuwa mkubwa. Hata hivyo mfalme alipoulizia habari za mtoto Yesu kuzaliwa, ilionekana
kuwa mfalme alitabiriwa kuzaliwa humo
Bethlehemu. Ingawa Bethlehemu ilionekana kama mji mdogo, tena wa kudharaulika, maisha duni
lakini kwa kupitia nyota ya Yesu, mji
huu ukapata heshima. Nyota ya mji ikionekana, maendeleo yatatokea. Inahitajika nyota ya mtu mmoja.
Nyota ya mtu mmoja tu inaweza kubadili historia ya mji wote
na kufuta historia za maisha marefu ya kudharauliwa katika Jina la Yesu.
3. Nyota ikionekana hazina huwa
zinafunguliwa: Imeandikwa MATHAYO 2:10-11… [Nao walipoiona ile nyota, walifurahi furaha kubwa mno. 11 Wakaingia
nyumbani, wakamwona mtoto pamoja na Mariamu mamaye, wakaanguka wakamsujudia;
nao walipokwisha kufungua hazina zao, wakamtolea tunu; dhahabu na uvumba na
manemane.]…Hazina huwa zinafunguliwa pale mwenye nyota
akipatikana. Wapo wanaong’ang’ania wafanikiwe, lakini haitokei kwa sababu nyota
zao hazijaonekana. Ndoa zitapatikana, watoto watazaliwa pale.
4. Nyota ikionekana utafanikiwa na
kuheshimika: Wale wasiokufahamu wataanza
kukufahamu. Mamajusi walikuwa hawafahamu Bethlehemu. Lakini kupitia hii nyota,
walifanikiwa kupajua. Hata mama yake Yesu aliweza kufahamika kwa sababu ya Yesu
kuzaliwa. Mamajusi walisujudu, kwa sababu ya nyota ya Ufalme wa Yesu. Nyota ikipatikana, watu
watakuja wenyewe na kusujudu hata nchi, na heshima yako itakurudia kwa Jina la
Yesu. Nyota huwavuta watu watoke walipo ili kukufuata wewe.
5. Nyota huleta mwangaza na kufanikiwa
kwa mtu: Imeandikwa katika ISAYA 60:5-6 …[Ndipo utakapoona na kutiwa nuru, Na moyo wako utatetemeka na kukunjuka;
Kwa kuwa wingi wa bahari utageuzwa kukujia, Utajiri wa mataifa utakuwasilia. 6
Wingi wa ngamia utakufunika, Ngamia vijana wa Midiani na Efa; Wote watakuja
kutoka Sheba; Wataleta dhahabu na uvumba; Na kuzitangaza sifa za Bwana.]….Nyota
yako ikeshaonekana utajiri na mafanikio
yatakujia yenyewe kutokea mbali.
UKIRI
Kuanzia
leo ninahitaji nyota, kwa Jina la Yesu. Ewe nyota ya heshima uliyekwama
mahali popote ninakulazimisha kwa Damu ya Yesu njoo, njoo, njoo, kwa Jina la
Yesu. Ewe nyota wa kufahamika na kuheshimika uliyezuiliwa na waganga wa
kienyeji na wachawi nakuita njoo, kwa Jina la Yesu. Amen
|
DALILIZAMTUALIYEIBIWA NYOTA
1. Kila utakachokifanya kitakosa ufanisi:
Mtu wa aina hii hukosolewamara zote badala ya kupongezwa kwa kazi anayoifanya.
2. Mtu hufanya mambo Kwa uzito kwa
ugumu: Kama ni biashara hata uitangaze redionina magazetini,
utatumianguvu nyingi sana. Mara nyingine mtu huyo huzunguka hapa na pale
akitafuta mafanikio yake lakini haimsaidii. Mtu wa aina hii hujikuta akikiri
‘maisha ni magumu’
3. Kila anachokifanya hakifiki kwenye
mafanikio yake: Mathalani endapo ni biashara,
huishia kuwa hasara na kuacha.mwingine huacha kazi.
TAHADHARI YA NYOTA:
Nyota
ikishaonekana kuna watakainuka na wengine kuanguka: Kuna wengi utakaowainua na
wengine utakuja kuwapoteza. Simeoni
baada ya kumpokea Yesu mikononi
mwake alisema maneno haya, katika LUKA
2:34...[Simeoni
akawabariki, akamwambia Mariamu mama yake, Tazama, huyu amewekwa kwa kuanguka
na kuinuka wengi walio katika Israeli, na kuwa ishara itakayonenewa.]…
Wapo ambao ni rafiki zako wanaweza
kukuacha nyota yakoikionekana.
UKIRI
Kuanzia
leo,na kuanzia sasa, Nitaishi sawasawa na nyota yangu kwa Jina la Yesu. Mtu
yeyote unayezuia nyota yangu, leo nashambulia kazi yako, niachie kwa Kwa Jina
la Yesu.Wewe unayetumia nyota yangu, niachie kwa Jina la Yesu.Naweka uhuru
kuanzia leo.ninaamuru kuanzia leo, na kuanzia sasa wale wanaotumia umahiri
wako, wayaachie maisha yako kwa Jina la Yesu. Ewe nyota yamafanikio
uliyefichwa mahali popote nakuamuru
njoo kwa Jina la Yesu. Amen.
|
Endapo mtu hujaokoka, leo ni siku muhimu kwako
kufanya uamuzi huo. Hii itakusaidia kwamba asiwepo mtu yeyote atakayeiiba nyota
ya maisha yako.
=== © Information & Media Ministry ===
(Ufufuo Na Uzima -
Morogoro)
Mtaa wa Nguvu Kazi,
(Minara Mitatu), Mkundi-Morogoro.
/or
Contact our Church
Leadreship:
Bishop Dr. Godson Issa
Zacharia
(Glory of Christ
(Tanzania) Church in Morogoro).
Cellphone: (+255)
765979866 /or +255 713459545.