Na: BRYSON LEMA (RP)
Utangulizi:
Historia ya Ukristo inaonesha kuwa ulianza kwa vurugu, na bila vita Ukristo haupo. Kila mtu ana
historia yake. Katika maisha ya kila siku,yapo mambo uliyotaka kuyafanya
lakni hujaweza kuyafanya, pengine kwa kukosa uwezo, au kukosa watu wa kukusaidia kufanya hivyo.
YOHANA 5:2-6..[Na huko Yerusalemu penye
mlango wa kondoo pana birika, iitwayo kwa Kiebrania Bethzatha, nayo ina matao
matano. 3 Ndani ya hayo jamii kubwa ya wagonjwa walikuwa wamelala, vipofu,
viwete, nao waliopooza, [wakingoja maji yachemke. 4 Kwa maana kuna wakati
ambapo malaika hushuka, akaingia katika ile birika, akayatibua maji. Basi yeye
aliyeingia wa kwanza baada ya maji kutibuliwa, akapona ugonjwa wote uliokuwa
umempata.] 5 Na hapa palikuwa na mtu, ambaye amekuwa hawezi muda wa miaka
thelathini na minane. 6 Yesu alipomwona huyu amelala, naye akijua ya kuwa
amekuwa hali hiyo siku nyingi, alimwambia, Wataka kuwa mzima?]… Unapoangalia maisha yako, unaona kwamba kuna kitu unachokihitaji ili
uingie mahali fulani. Wakati mwingine zipo sababu au watu waliofanya wewe uwe
kama ulivyo: waliosababisha ndoa kukosa amani, uwepo wa magonjwa,
kutokusoma, kufukuzwa nyumbani n.k. Wanadamu mara zote hupenda kupeleka
lawama zao kwa wale waliosababisha maisha yao kuwa jinsi yalivyo.
Yusufu ni miongoni mwa watoto 12 wa Yakobo. Ndugu zake Yusufu walimchukia
sana,kwa kuwa Baba yao alimpenda sana
Yusufu kuliko wao, na hata akamshonea mavazi yenye rangi tofauti na wao. Wakati Yusufu
anawahadithia ndugu zake ndoto alizo nazo, wao kumbe jambo hilo lilikuwa linawaumiza ndugu zake. Baadae kaka zake wakapanga kumuua ili
ndoto za Yususu zisitimie.
Siku moja Baba yao alimtuma Yusufu kwenda kuwaangalia ndugu zake wakiwa malishoni, na walipomuona kwa mbali wakaweka kikao cha ghfala cha kumuua Yusufu. Bila yeye kujua, Yusufu alikamatwa na ndugu zake wakamtupa shimoni. Hata hivyo, Mungu alikuwa upande wake. Mungu alijua kuwa bila Yusufu kuuzwa Misri, siyo rahisi kwake kutawala. Yusufu akiwa Misri zile ndoto haoti tena, hamsikii Mungu akiongea naye tena. Aliwekwa jela kwa kesi ya kusingiziwa, na humo gerezani alijua ndiyo mwisho wa maisha yake.
Siku moja Baba yao alimtuma Yusufu kwenda kuwaangalia ndugu zake wakiwa malishoni, na walipomuona kwa mbali wakaweka kikao cha ghfala cha kumuua Yusufu. Bila yeye kujua, Yusufu alikamatwa na ndugu zake wakamtupa shimoni. Hata hivyo, Mungu alikuwa upande wake. Mungu alijua kuwa bila Yusufu kuuzwa Misri, siyo rahisi kwake kutawala. Yusufu akiwa Misri zile ndoto haoti tena, hamsikii Mungu akiongea naye tena. Aliwekwa jela kwa kesi ya kusingiziwa, na humo gerezani alijua ndiyo mwisho wa maisha yake.
Yamkini wewe unaweza kusema hajawahi kutupwa shimoni kama Yusufu na kwa hiyo hili somo halikuhusu.
Kumbuka kwamba, "Agano la Kale ni la mwilini", lakini "Agano Jipya ni la rohoni".
Si ajabu wapo ndugu zako ambao wamekwisha kukuweka shimoni kama Yusufu (katika ulimwengu
wa roho) lakini wewe upo tu bila kufahamu kinachoendelea rohoni.
Shetani lazima ajue kuwa ile miaka aliyoiiba kwako atairudisha yote.
Farao aliyekuwa anawazuia Israeli wasiondoke, hatimaye ndiye huyo huyo aliwaambia
waondoke na chochote wanachokitaka, ikiwemo mali na dhahabu za Wamisri. Wana wa Israeli hawakuishia jangwani bali
walifika Kanaani, maana Bwana wa Mabwana
alisema, na "yeye si mwanadamu hata aseme uwongo". Ndugu za Yusufu walitummika ili
kumfikisha Yusufu kwenye hatima ya ndoto yake ya kutawala. Yusufu hakuwachukia
ndugu zake. Hata wewe wale
waliokuharibia maisha yako,usiwachukie kwa sababu Mungu aliwaweka mahsusi kwa ajili ya kuinuiliwa
kwako.
MWANZO
45:1-8..[Hapo
Yusufu hakuweza kujizuia mbele yao wote waliosimama karibu naye. Akapiga
kelele, na kusema, Mwondoeni kila mtu mbele yangu. Wala hakusimama mtu pamoja
naye, Yusufu alipojitambulisha kwa nduguze. 2 Akapaza sauti yake akalia, nao
Wamisri wakasikia. Watu wa nyumba ya Farao nao wakasikia. 3 Yusufu akawaambia
ndugu zake, Mimi ndimi Yusufu; baba yangu angali hai bado? Wala ndugu zake
hawakuweza kumjibu, maana waliingiwa na hofu mbele yake. 4 Yusufu akawaambia
ndugu zake, Karibuni kwangu; basi, wakakaribia. Akasema, Mimi ni Yusufu, ndugu
yenu, ambaye mliniuza kwenda Misri. 5 Basi sasa, msihuzunike, wala msiudhike
nafsi zenu, kwa kuniuza huku; maana Mungu alinipeleka mbele yenu kuhifadhi
maisha ya watu. 6 Maana miaka hii miwili njaa imekuwa katika nchi, na iko tena
miaka mitano isiyo na kulima wala kuvuna. 7 Mungu alinipeleka mbele yenu
kuwahifadhia masazo katika nchi, na kuwaokoa ninyi kwa wokovu mkuu. 8 Basi si
ninyi mlionipeleka huku, ila Mungu; naye ameniweka kama baba kwa Farao, na
bwana katika nyumba yake yote, na mtawala katika nchi yote ya Misri.]… Bila ndugu zake Yusufu kumuuza Misri, leo hii historia ya Yusufu isigekuwa
inafahamika. Hakuna Samweli bila Penina.
Pale Penina anapoinuka, Samweli huzaliwa.
Wale waliokuinukia ni kwa ajili
ya ushindi wa maisha yako.
Hapa juu ni Vijana wa Showers of Glory kama kamera yetu ilipowanasa wakiimba na kumchezea Bwana wa Mabwana wote, Mungu Mkuu kuliko miungu yote - Jumapili 19/4/2015. |
Wewe ambaye hujaokoka, ni vyema leo kufanya hayo maamuziilikumpata Mungu
aliye mkuu kulikomiungu yote anayewatoa watu gerezani na kuwaweka katika
utawala.
Mtaa wa Nguvu Kazi,
(Minara Mitatu), Mkundi-Morogoro.
/or
Contact our Senior
Pastor:
Dr. Godson Issa Zacharia
(Ufufuo Na Uzima – Morogoro)
Cellphone: (+255) 757
550878 / +255 719798778