Sunday, June 7, 2015

SILAHA ILIYOANDALIWA KUNIANGAMIZA-Na: BRYSON LEMA (RP)


JUMAPILI:  07 JUNE 2015 - UFUFUO NA UZIMA MOROGORO

 
Utangulizi:Tunaposema silaha,  wengi wetu wanawaza sime, bunduki, mishale n.k. Mwindaji anapokuja kwako, huja akiwa na silaha. Imani yake mwindaji ni kuwa,  kwa silaha aliyoibeba,  wewe hutapita. Hata hivyo, Mungu  wetu naye ameandaa silaha. Tatizo kubwa hapa ni kuwa, silaha ya Mungu haionekani, kwa sababu Mungu wetu hubadilisha kitu kulingana na matumizi.  Mungu akimaua kugeuka sime,anafanya hivyo.

 

AMOSI 3:5..[Je! Ndege ataanguka mtegoni juu ya nchi, mahali asipotegewa tanzi? Mtego utafyatuka juu ya nchi, bila kunasa kitu cho chote?]…. Hii ina maana kuwa, umuonapo ndege kanaswa katika mtego, ujue kuna aliyeutega. Kila kitu na mtego wake, na kila silaha na mtu wake. Mtego wa ndege haumasni swala, na mtego wa swala haumnasi nyani.

 

Katika maisha ya kawaida, ipo mitego na pia wapo wawindaji.  Katika Biblia, shetani anaonekana akizuia Ibrahimu asipate uzao kupitia Sarah, kwa kuwa alishajua kupitia uzao wa Ibrahimu Baraka za Mungu zitafuatana na uzao wake. Shetani alitengeneza silaha za kumzuia Ibrahimu kupata motto, bila yeye na mkewe kujua. Mwishowe, baada ya  kukata tama kwa muda mrefu, hatimaye alipata mtotoo aitwae Isaka. Hata hivyo Isaka naye alipitia kipindi kigumu kama hiki cha Ibrahimu, kwa sababu tumbo la mkewe nalo lilifungwa asizae.

 

Hata uhai ulio nao ni sehemu ya miujiza.  Kumbuka kuwa,  Bwana amekupitisha katika  nyakati usizozijua na kukuepusha na mitego mingi  sana ya wawindaji. Kila jambo ulionalo maishani mwako lina sababu yake. Kwa kadiri unavyopiga hatua za maisha yako,  ujue kuna ………….

 

Kupitia Isaka, shetani aliwachonganisha Yakobo na Esau. Kupitia Yakobo, shetani alisababisha asimuoe Raheli kwa sababu alishaona ndani  ya tumbo la Raheli angepatikana Yusufu, yaani mkombozi wa wana wa Israeli, atakayewaokoa wasife kwa njaa. Hata baada ya Yusufu kuzaliwa,  shetani alitengeneza mipango mibaya ili Yusufu asifikie ndoto zake. Yusufu alitengenezewa mipango mibaya, pale ndugu zake walipomuuza kwa wafanyabiashara wa Kimisri. Kumbuka lengo  la shetani  siyo Yusufu auzwe Misri bali auae na afe. Hata Yusufu alipokuwa Misri, bado shetani aliendelea kuandamwa na shetani kiasi kwamba alitupwa gerezani, na hapo ikawa ndio mwisho  wa ndoto zake.

 

Yusufu akiwa gerezani, ndiposa Farao akota ndoto ambayo haikupata mtafsiri bali kwa kupitia kwa Yusufu peke yake. Yusufu alipotoka gerezani alienda moja kwa moja kuwa mtawala wa nchi ya Misri. Bwana atafungua mlango kwako

 

Baada ya Yusufu kuimaliza kazi yake ya ukombozi, alilala na baba zake. Mwanzoni mwa Kitabu cha Kutoka, habari za Mfalme mpya wa Misri asiyemjua Yusufu  zinaelezwa. Kila  vita husimama kwenye  kila hatua. Wazalishaji wa Kimisri wanaelekezwa wasiachie Waisrael kujifungua salama, na ikitokea hivyo, watoto  wa kiume wote wauae‼ Kumbe aliyekuwa anawindwa hapa ni Musa,  ili   Israeli wasipate mtu wa kuwaongoza watoke utumwani. Hata wazazi wa Musa nao walishindwa jinsi  ya kumlinda, na kuazimia kumweka kando ya mto  na papo hapo Bwana akatengeneza njia ya kumuokoa. Kumbe basi, wanaddamu hufika mwisho na wakawa hawawezi.  Lakini ugumu wa wanadamu siyo ugumu wa Mungu Baba.

 



Usikate tamaa. Yamkini upo mahali ambapo madaktari wamekuambia ugonjwa ulio  nao hauna tiba,  lakini Bwana Yesu yupo kwa ajili ya shida yako, naye atafanya safina katika mito ya Misri. Kumbuka mwisho wa wanadamu ni  mwanzo wa Mungu. Katikati ya maadui, Musa alikuzwa na kukua. Musa alikula mbele ya Farao, na  kukulia ndani ya nyumba ya Farao. Mbinguni Mungu alikuwa akijua huyu ndiyo mbabbe wa Farao.  Musa akakua katikati ya adui zake. Daudi akasema, “Bwana huandaa meza mbele zangu,  machoni pa watesi wangu”. Ambacho Wamisiri hawakukijua ni kuwa, Musa ni kutoka juu na yupo kwa kazi maalumu. Kuku ni kuku,hawezi kuwa tai hata siku moja.

 

Musa alikimbilia jangwani ili  kujifunza mbinu za kuishi jangwani. Shetani alidhani kuwa Musa akiwa jangwani hatoweza tena kuwakomboa Israeli. Hata hivyo  ndani  ya jangwa alikokimbilia kwa kuitwa muuaji, ndiko huko huko alipokutana na kichaka chenye kutoa sauti.  Musa alipotoka jangwani, kwenda kwa Farao kwa kazi maalumu,  hakwenda kama yule Musa wa zamani, bali alikuwa kama jemedari aliyepata mafunzo.

 

Muda usingetosha ningekuletea habari za Joshua,  Esta, Gideon, Samsoni na Waamuzi mbalimbali wa Israeli. Cha kujua hapa ni kuwa, Bwana kwa kila mmoja wao,  alifanya njia pasipo njia. Daudi mathalani,  katika wana wa familia ya Yese, hakuonekana wa maana, na ndiyo maana wakati Samweli  anasubiri ampake mafuta, Yese alikuwa kasahau kabisa kuwa yupo mwanane mwingine ambaye hajatokezea. Ndiposa Bwana akamwambia Samweli, kuwa asimpake mafuta Eliabu wala wana wengine wa Yese kwa sababu Mungu haangalii kama vile wanadamu wanavyoangalia. Usiogope upitapo katika bonde la uvuli wa mauti, kwa sababu Bwana yupo ili  akupiganie. Hutakufa wala hutaangamia,bali utaishi  katika ushindi  wote.

 

ISAYA 49:1-2..[Nisikilizeni, enyi visiwa; tegeni masikio yenu, enyi kabila za watu mlio mbali sana; Bwana ameniita tangu tumboni; toka tumbo la mama yangu amenitaja jina langu. 2 Naye anifanya kinywa changu kuwa kama upanga mkali; katika kivuli cha mkono wake amenisitiri; naye amenifanya kuwa mshale uliosuguliwa; katika podo lake amenificha;]…. Kumbe jina nililo nalo,  hakunipa baba au mama yangu. Hili ni  jina alilonipa Bwana, na wazazi wakatumika tu kukamilisha mpango wa Bwana. Wengine wananiona mimi kama mshale, na gari la vita la Bwana. Kumbe yale magumu adui zangu mnayoileta kwangu ni kutetemeka kwenu. Mimi  sikujua adui zangu wanatetemeka wanionapo. Kumbe adui wanapokuja na silaha zao kwangu ni kwa sababu wanaziona silaha nilizo nazo mimi. Kumbe mimi ni silaha za Bwana, ndiyo maana adui zangu wanatetemeka na kufuatilia maisha yangu wanaponiona.  Kama ulifikiri ndoa yangu ilianzia hapa duniani ujue umekosea, kwa sababu tangu nikiwa tumboni nilishafanywa silaha za Bwana za vita. Mwenye nyundo au rungu ndiye anayeibeba na kuichomoa ili  apige maadui zake. Imeandikwa “mimi ni rungu la Bwana na silaha za Bwana za  vita”. Kwa hiyo Bwana mwenyewe hukutumia wewe kuwapiga wachawi na wanaotumia  nguvu za giza kutawala. Bwana amesema “Bwana ni mtu wa vita, Bwana ndilo Jina lake”. 

 

Ni saa ya kuwapiga walioharibu maisha yako. Usimuogope yule aliyekuja kufanya vita na wewe. Ukiona unapigwa vita ujue tayari umemzidi adui yako. Jua kuwa kama ungekuwa hujamzidi  asingefanya vita na wewe. Hata hivyo ili uweze kupigana ni lazima Yesu Kristo awe ndani  ya moyo wako.


Endapo wewe hujaokoka, leo ni sikumuhimu kwako kufanya maamuzi ya kuokoa na ndipo uewze kupigana na adui wanaowinda maisha yako na  kuwa mshindi katika Jina la Yesu. 

                          © Information Ministry (Ufufuo Na Uzima - Morogoro)

Mtaa wa Nguvu Kazi, (Minara Mitatu), Mkundi-Morogoro.

 /or

Contact our Senior Pastor:

 Dr. Godson Issa Zacharia

 (Ufufuo Na Uzima – Morogoro)

Cellphone: (+255) 765979866 /or +255 713459545

 

Share:

Related Posts:

Powered by Blogger.

Pages